Sunday, June 16, 2013

Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
Lejendari wa timu ya taifa ya Ufaransa na klabu ya Real Madrid ambaye kwa sasa ni mkurugenzi wa michezo wa miamba hiyo ya Hispania, Zinedine Zidane amemuomba mshambuliaji nyota wa klabu ya kaskazini mwa London, Tottenham Hospur, Gareth Bale kuiambia klabu hiyo kuwa anataka kuondoka ili kuongeza kasi ya dili la kusajiliwa Santiago Bernabeu.
 Zidane amepewa kazi ya kuhakikisha wanamnasa mchezaji huyo hatari ambaye ni chaguo namba moja kwa miamba hiyo ya soka la Hispania.
Taarifa kutoka Spurs zinaeleza kuwa Bale mwenye umri wa miaka 23 kwa sasa, bado ana furaha ya kuwepo White Hart Lane licha ya timu yake kushindwa kufuzu kucheza ligi ya mabingwa barani ulaya mwakani.
Lakini Zidane anaamini kuwa Bale kujiunga na miamba hiyo yenye mafanikio barani ulaya itakuwa vizuri kwake, hivyo ailazimishe klabu yake kumuuza katika majira ya joto ya usajili.
“Nadhani Real Madrid imevutiwa na Bale, hilo halina ubishi kabisa, na klabu haina shaka na ada ya usajili, ipo tayari kumwaga kitita kikubwa ili kumnasa nyota huyo”. Zidane ameliambia gazeti la Sunday.
Zidane ameongeza kuwa kama Bale anafikiria kuwa ni muda wake kuhama, basi aongee na viongozi wa klabu yake ili taratibu zikamilike.
Real deal? Madrid have made no secret of their desire to sign the winger 
Real Madrid wamekufa wameoza kwa nyota huyu ambaye msimu uliopita alitwaa tuzo mbili za uchezaji bora nchini EnglandHot property: Bale is one of the most sought-after players in Europe 
Mali ya moto: Bale ni chagua la kwanza la usajili wa Real Madrid
Mapema wiki hii, mchezaji wa zamani wa Tottenham Luka Modric alikaririwa na vyombo vya habari kuwa Bale ataendana na mfumo wa Real Madrid, hivyo akubali kujiunga nao.
All smiles: Bale visits Universal Studios in Florida this week

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video