Wednesday, May 1, 2013

image61

Na Baraka Mpenja
Ligi kuu soka Tanzania bara imeendelea leo katika miji ya Dar es salaam, Pwani na mji kasoro bahari Morogoro Tanzania.
Jijini Dar es salaam zimepigwa mechi mbili ambapo mabingwa wa ligi hiyo klabu ya Yanga imewakaribisha Wagosi wa Kaya Coastal unioni ya jijini Tanga na kushuhudia dakika tisini za mchezo huo zikimalizika kwa sare ya kufungana bao 1-1.
Sasa Yanga wanasubiri mechi ya mwisho dhidi ya watani zao wa jadi, wekundu wa Msimbazi Simba “Taifa kubwa” itakayopigwa mei 18 uwanja wa taifa Dar es salaam.
Huko Chamazi maafande wa JKT Ruvu waliwakaribisha maafande wa Tanzania Prisons ya jijini Mbeya na mtanange huo umemalizika kwa Prisons kuibuka kidedea baada ya kushusha kipigo cha mabao 2-1 na kupanda mpaka nafasi ya 8 na pointi 29, sasa hawashuki daraja tena.
Mkoani Morogoro katika dimba la Jamhuri, vibonde wengine wa ligi hiyo Polisi Morogoro chini ya kocha Rishard Adolf wamewakaribisha Kagera Sugar na kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya vijana wa Abdallah Kibaden “King Mputa” na kusubiri hatima ya JKT Ruvu ambao leo pia wamepigwa chamazi.
Huko Mashamba ya miwa Manungu Turiani mji kasoro bahari, wakata miwa wa Mtibwa sugar walishuka dimbani dhidi ya vibonde wa ligi hiyo Africa Lyon ambapo Mtibwa wameibuka kifua mbele kwa ushindi wa mabao 2-0 huku mabao yote yakitiwa kimiani na nyota  wao aliyerejea baada ya kuwa majeruhi, Hussein Javu.
Na huko Mabatini Mlandizi mkaoni Pwani, wanajeshi wa Ruvu Shooting walipambana na wanajeshi wenzao wa JKT Oljoro na mechi hiyo kumalizika kwa suluhu pacha ya bila kufungana.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video