Tuesday, May 7, 2013

Waziri-Mkuu-Mizengo-Pinda
 Na Magreth Kinabo – Maelezo
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amelipongeza Jeshi la Polisi nchini katokana  na juhudi mbalimbali linalozionesha na kuwataka wabunge  kulitia moyo.
Kauli hiyo ilitolewa leo Bungeni na Waziri Mkuu Pinda mara baada ya kuwasili mjini Dodoma akiwa ametokea  jijini Arusha baada ya kuwatembelea majeruhi waliolazwa kwenye Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru, jijini Arusha ili kuwajulia hali.
Majeruhi hao walilazwa katika hospitali hiyo kufuatia mlipuko wa bomu ulitokea lipuko wa uliotokea katika kanisa la katoliki la Mtakatifu Joseph  Parokia ya Olasiti  Arusha   Mei 5, mwaka huu saa 4:30  na kusababisha vifo vya watu  watatu na majeruhi 69.
” Jana lilikuwa ninasiliza mjadala wa Bunge nimesikia jeshi la polisi likiwa linalaumiwa. Chombo hiki kinajitahidi … tuwatie moyo tuwatie nguvu .Serikali itaendelea kuwasaidia,” alisema Waziri Mkuu Pinda.
Kauli hiyo pia iliungwa mkono na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera,Uratibu wa Bunge William Lukuvi  wakati akichangia mjadala wa Makadrio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2013/2014.
Wabunge wengine waliopongeza jeshi hilo , wakati wa mjadala huo ni Richard Ndassa  Mbunge wa Jimbo la Sumwe- CCM, ambaye alisema  kama kusingewepo na juhudi za polisi na uwepo wao  wanaotuhumiwa  katika tukio la Arusha  wasingekamatwa.
Huku akimshauri Spika wa Bunge la Jamhuri ya   Muungano wa Tanzania, Anne Makinda kuwa   katika maeneo ya nyuma ya jengo la Bunge kwenye maegesho yaimarishwe ulinzi.
“Nawatia moyo polisi … wanafanya kazi ngumu tunapowabeza hatuwatendei haki,” alisema.
Naye Aggrey   Mwanri, ambaye ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Mbunge wa Jimbo la Siha, alisema jeshi hilo linafanya kazi vizuri hivyo kinachotakiwa ni ushirikiano kutoka kwa wananchi.
Kwa mujibu wa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utawala Bora, Kapteni George Mkuchika alichangia mjadala huo alisema jeshi askari polisi mmoja huduhimia raia 1:1100 , twakimu za mitaifa zinaoyesha askari polisi 1:400-600.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video