Tuesday, May 21, 2013

Daniel na Mwalimu – Timu pekee kutoka Tanzania iliyobaki katika mashindano ya Guinness Football Challenge, Mwalimu Akida(kulia) na Daniel Msekwa(kushoto) tayari kwa nusu fainali ya kesho Larry&Mimi
 Mei 15, 2013 Dar es Salaam, Jumatano iliyopita kupitia televisheni za ITV na Clouds TV timu ya Ghana iliyoshinda katika kipindi cha Tisa cha GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE walifurahia kupata nafasi katika nusu fainali kwa kucheza azonto ambayo iliwafanya watangazaji Larry na Mimi kujiunga nao. Kofi Okarku na Isaac Aryee ingawa hawakufanya vizuri katika hatua ya mwisho ya ukuta wa pesa wa Guinness walifanikiwa  kupata  dola za kimarekani 1,500 na waliufanya uwanja wote kunyanyuka na kucheza.
 Timu iliyoshinda ilifanya vizuri katika hatua za mwanzo na kujipatia alama 16 pamoja na kuonesha uwezo mzuri ufahamu wa soka. Waliwashinda Wakenya katika hatua ya penati, hata hivyo timu ya Kenya imefuzu nusu fainali kama washindi wa pili.
 Emanuel, Kenneth, Chris na Isaac wataendelea kuziwakilisha nchi zao katika hatua ya nusu fainali, wakiwa na ndoto za kufanya vizuri na kuwa  washindi wa Pan-African Guinness Football Challenge.
 Meneja wa kinywaji cha Guinness Davis Kambi alisema, “Nusu fainali ya kwanza inatarajia kufanyika wiki ijayo tukisubiri kuona ni nani atakayefanikiwa kutinga fainali ya GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE. Timu kutoka Dar-es-Salaam,Daniel Msekwa na Mwalimu Akida Hamad watapeperusha bendera ya taifa letu na kuwakilisha Afrika mashariki hivyo  tunawatakia kila la heri. Tunazisifu timu zote na sasa timu bora zitakutana kuwania kufuzu kuingia fainali”
 Timu zitakazoendelea na michuano ni pamoja na;
KWA WATANZANIA
  • NDANI YA JEZI ZA KIJANI-Kutoka Dar-es-Salaam, Daniel Msekwa na Mwalimu Akida Hamad ambao awali  walijishindia dola za kimarekani  5,500 katika mashindano ya kitaifa na waliishia katika hatua ya penati kwenye robo fainali wataweza kufikia hatua ya pesa ukutani katika nusu fainali?
 KWA WAKENYA
  •  NYEUSI-Kenneth Kamau na Wills Ogutu wote kutoka Nairobi.Ken ni kocha na Wills ni dereva.Timu hii ilijishinda katika robo fainali ya pili na kuongeza  dola 1,500 kwenye dola 3,000 walizokuwa nazo awali.
  • JEZI NYEKUNDU-ni timu ya pili kutoka Kenya,Francis Ngigi kutoka Nairobi na Kepha Kimani kutoka Thika.Timu hii ilipata dola 3,000 katika hatua za kitaifa na walifika hatua ya penati katika robo fainali.
 KWA WAGHANA
  • JEZI ZA BLU- Timu ya Ghana iliyopata fedha nyingi zaidi katika hatua ya kitaifa, Jonathan Naab kutoka Tindogo na Desmond Odaano kutoka Larteh wamefanikiwa kufika hatua ya nusu fainali baada ya kupata jumla ya dola 8,500. Je, watafanikiwa kuingia fainali?
 Nusu fainali ya kwanzaitarushwa na televisheni za ITV na Clouds TV usikose kuangalia mchezo huu na kushangilia timu yetu.
  Wapenzi wa kipindi hiki cha Guinness football challenge nchini wanaweza kupima maarifa yao katika soka kupitia GUINNESS® VIP™.  Wanaweza kufanya hivyo kwa kujisajili bure kabisa katika m.guinnessvip.com kwa kupitia simu ya mkononi.  
 Usikose kuufwatilia ukurasa wa facebook wa GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE kwa habari mbalimbali.
-www.facebook.com/guinnesstanzania
 GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE, ni kipindi cha mchezo wa soka kinachotayarishwa na kampuni ya kimataifa ya Endemol.  Usikose kuangalia na kufuatialia kipindi hiki katika runinga yako kupitia televisheni za ITV na Clouds TV kila siku ya Jumatano usiku saa 3:15 ITV na saa 2:15 Clouds TV.
 Usisahau kuwa na chupa ya bia uipendayo ya Guiness wakati unaangalia kipindi hiki. 
 Tafadhali kunywa kistaarabu- Hairuhusiwi kuuzwa kwa wale wenye umri chini ya miaka 18.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video