Friday, May 17, 2013


MAZOEZI 
Nyota wa Simba wakipasha misuli kujiandaa na kipute cha kesho cha watani wa jadi katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam. Kocha Mfaransa Patrick Liewig ataoneshana kazi na Mholanzi Ernie Mazoezi-ya-YangaWanajangwani Dar Young Africans wakiweka miili sawa kwa ajili ya kuwakabili Simba waliowapiga mabao 5-0 msimu uliopita, hakika mzimu huu unawasumbua sana Yanga
ernestbrandts 
Maarifa ya Mholanzi Ernie Brandts mbele ya maarifa ya Mfaransa wa Simba Patrick Liewig Patrick-Liewig 
Patrick Liewig kuiongoza Simba kesho uwanja wa taifa kuwatafuna Yanga

Na Baraka Mpenja
Ilikuwa inahesabika miezi, wiki, siku na sasa imebaki siku moja tu kushuhudia watani wa jadi, yaani wekundu wa Msimbazi Simba “Taifa Kubwa” wakigagaduana vikali na mabingwa Dar Young Africans katika uwanja wa kisasa wenye sifa zote wa taifa jijini Dar es salaam “Jiji la maji chumvi”  kesho majira ya saa 10 kamili jioni.
Kiputo hicho kinatarajiwa kuwa na burudani kubwa kutokana na uwezo mkubwa wa wachezaji wa miamba hii ya soka la Tanzania.
Simba chini ya kocha Mfaransa Patrick Liewig akisaidiwa na kocha mzalendo aliyebarikiwa kuwa na maneno mengi  Jamhuri Kiwhelu “Julio Alberto” wanatumia vijana zaidi kuliko wachezaji wakongwe “Mafaza” na hii imesababisha klabu hiyo kuwa na kikosi chenye makali zaidi hususani mechi za lala salama, lala kwa buriani za ligi kuu.
Yanga wao wamechangaya damu kuna mafaza wengi na vijana, lakini ni kikosi ambacho kinasemekana kukamilika zaidi, ndio maana kimeweza kuwapokonya watani wao wa jadi mwari wa ligi hiyo.
Wakati Kelvin Yondan, Mbuyu Twite, Oscar Samwel Joshua, Nadir Haroub “Canavaro” wakisimama katika ukuta wa Yanga, vijana wa Simba, Haruna Chanongo, Ramadhan Singano “Messi”, wakiongozwa na Mrisho Khalfan Ngasa watakuwa wanatafuta maarifa ya kupenya na kumtafuta kipa nambari moja wa Yanga aliyeitwa Taifa Stars na kukutana na mpinzani wake kwa mara nyingine Juma Kaseja ambaye alimuweka benchi muda wote wakiwa Simba, namzungumzia Ally Mustapha “Bartez”.
Katikati ya dimba itakuwa burudani kubwa sana wakati Amri Athman Kiemba, Jonas Mkude, Musa Mude, Mwinyi Kazimoto watakuwa wanapambana na akina Athman Idd “Chuji”, Haruna Hakizimana Fadhil Niyonzima “Fabrigas”, na Frank Domayo.
Ngasa ataichezea Simba mbele ya timu yake kipenzi ya Yanga, wakati akipangwa kuongoza mashambulizi ya Simba akitokea winga ya kulia, kwa upande wa Yanga, kijana mdogo anayehofia urejeo wa Ngasa jangwani, Simon Msuva atakuwa anakimbiza upande wa kulia akipiga krosi ndani ya eneo la sebule la Simba na kukutana na Didier Kavumbagu, Jerryson Tegete, Khamis Kiiza “Diego” wanaotarajia kusimama sehemu ya mashambulizi.
Tayari maandalizi ya mechi hiyo ya watani wa jadi yamekamilika kwa mujibu wa viongozi wa timu hizo.
Afisa habari wa Yanga akiwa Pemba visiwani Zanzibar, Baraka Kizuguto ameimbia MATUKIO DUNIANI  kuwa wamefanya maandalizi mazuri na wanajipanga kuingia Dar es salaam ili kutoa burudani katika mchezo wa kesho na kuibuka kidedea mbele ya Mnyama Pori.
“Sisi tumejiandaa vizuri ili kutoa burudani siku ya jumamosi, Yanga ni mabingwa lakini hiyo haituzui kutafuta ushindi mbele ya wapinzani wetu wakubwa katika soka la Tanzania, tuko fiti sana”. Alisema Kizuguto.
Kizuguto alisema kwa kawaida kocha wao Mholanzi Ernie Brandts siyo msemaji sana, ni mtu wa vitendo na ndio maana muda wote anashughulikia mazoezi kujiandaa na mchezo huo.
“Kwa mtu anayemfautilia kocha wetu, siyo msemaji sana ila ni mtu wa vitendo, amekiandaa kikosi kwa uzuri, mashabiki wa Yanga waje kwa wingi kushuhudia kikosi chao kilichotwaa ubingwa kikiwaadabisha Simba kesho”. Alitamba Kizuguto.
Akizungumzia hali ya wachezaji, Kizuguto alisema wachezaji wapo salama, hakuna majeruhi mpaka sasa ambaye yuko hatarini kuwakosa Simba na wana morali kubwa sana kuwakabili Simba hapo Kesho.
Alipoulizwa timu itawasili lini Dar es salaam, Kizuguto aligoma kueleza akidai Mechi za watani wa jadi huwa zina na fitina nyingi, lakini timu itakuwepo jumamosi uwanja wa taifa. MATUKIO DUNIANI  imebaini kuwa Yanga itawasili leo Dar es salaam na hii ni kwa mujibu wa kiongozi kigogo wa Yanga.
Wakati Yanga wakijinasibu kuibuka na ushindi, Simba kwa upande wao wamesema wapo tayari na wanasubiri kuwakabili wapinzani wao hapo kesho.
Mjumbe wa kamati ya usajili, mjumbe wa kamati ya utendaji, na mratibu wa timu katika mashindano, keptein wa zamani wa jeshi la kujenga taifa JWTZ , Zacharia Hans Poppe ameiambia MATUKIO DUNIANI kuwa wamekamilika na vijana wao wapo tayari kuwakabili wanaowaita wakongwe wa Yanga.
“Siku inawadia, kesho siyo mbali jamani, njooni  uwanja wa taifa ili muone kazi yetu, wakati wa maneno umekwisha”. Alisema Poppe.
Poppe alisema Simba bado wana wasiwasi mkubwa sana kufuatia TFF kubadilisha mwamuzi wa mchezo bila taarifa yoyote kwao, ila wameshaandika barua kwenda shirikisho wakiwataka waeleze sababu za kumuondoa Israel Nkongo na kumuweka Saanya wa Morogoro katika kipute hicho.
“Wenzetu toka mwanzo walikuwa wanamtaka mwamuzi huyo na wamempata, tutacheza kulingana na ufundi wetu na mambo yatakwenda salama”. Alisema Poppe.
Pia aliongeza kuwa mashabiki wa Simba wasiwe na wasiwasi hata kidogo, kikosi kipo shwari na vijana wao wana morali kubwa ya kuwanyoa Yanga bila kutia maji hapo kesho.
Mzunguko wa Kwanza wa ligi kuu soka Tanzania bara, miamba hiyo ilitoka sare ya bao 1-1, lakini kilio bado kipo kwa Yanga ambao msimu uliopita walipigwa kipigo cha aibu cha mabao 5-0.
Miongoni mwa wachezaji walioongoza kikosi cha simba kuwafunga Yanga walikuwa ni Emmanuel Okwi, marehemu “Mungu amlaze mahala pema peponi), Patrick Mutesa Mafisango, Ferlix Sunzu na nyuma alikuwepo Kelvin Yondan, sasa Sunzu pekee ndio yuko Simba mpaka sasa.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video