Tuesday, May 21, 2013

IMG_1656Na Lydia Churi- MAELEZO-DODOMA
Baadhi ya wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wameitakaSerikali kuharakisha kuulet
a bungeni Muswada wa Sheria ya Kusimamia Vyombo vya Habari ili kuhakikisha waandishi wa habari wanatekeleza majukumu yao kwa kufuata maadili na misingi ya taaluma hiyo.
Wakichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na  Michezo kwa nyakati tofauti, wabunge hao waliipongeza wizara hiyo kwa kuridhia Sheria ya Kusimamia Vyombo vya Habari kwa kuwa itasaidia kuikuza na kuiimarisha taaluma ya habari nchini.
Akichangia hotuba hiyo mbunge wa viti Maalum (CCM) Esther Bulaya alisema wakati umefika kwa waandishi wa habari nchini kuandika habari kwa kuzingatia maadili ya taaluma hiyo ikiwa ni pamoja na kuandika habari zilizofanyiwa utafiti wa kina na zinazohusisha pande mbili za chanzo cha habari.
Mhe. Bulaya  amewataka waandishi wa habari wasitumie vibaya uhuru wa habari kwa kutoa habari zinazoshabikia vyama vya siasa na zenye kuleta chuki zitakazowafanya vijana kujenga taifa la visasi. Aliongeza kuwa taifa ni zaidi ya vyama vya siasa.
Naye mbunge wa Kondoa Kusini, Mhe. Juma Nkamia alisema kupatikana kwa sheria ya kusimamia vyombo vya habari kutasaidia kuondokana na tatizo lililopo sasa la kuwa na waandishi wa habari wengi wasiokuwa na sifa maarufu kama ‘makanjanja’.  
Akizungumzia Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Nkamia aliitaka serikali kupitia wizara ya habari kuhakikisha inafanya kila liwezekanalo kuyamalizia majengo yaliyopo Mikocheni ambayo yametelekezwa kwa muda mrefu. Aliongeza kuwa majengo hayo yaliwekwa jiwe la msingi na Rais wa awamu ya pili Mzee Ali Hassan Mwinyi lakini mpaka sasa ni Serikali ya awamu ya nne na majengo hayo hayajakamilika.
Mhe. Nkamia pia aliitaka serikali kuiongezea bajeti TBC ili iweze kununua vifaa vipya na vya kisasa vya kurushia matangazo kwa kuwa vifaa vilivyopo vimechakaa. Aliongeza kuwa matangazo ya TBC hivi sasa hukatika katika kutokana na tatizo hilo.
Akiwasilisha hotuba ya Bajeti, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara aliliambia bunge kuwa serikali imeridhia kutungwa kwa Sheria ya Kusimamia Vyombo vya habari na muswada wa kutunga sheria hiyo utawasilishwa bungeni hivi karibuni.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video