Monday, May 20, 2013

Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
Kocha wa watukutu wa London, Tottenham Hospur, Mreno Andre Villas-Boas bado ana imani kubwa kuwa nyota wake na mfumania mabao wa klabu hiyo Gareth Bale atabaki White Hart Lane msimu ujao licha ya klabu hiyo kushindwa kufuzu kucheza ligi ya mabingwa barani ulaya.
Villas-Boas amesema nyota huyo anakodolewa macho na timu nyingi sana ili kumsajili, lakini bado Bale anaipenda Spurs na atabaki kuisaidia timu hiyo msimu ujao wa ligi kuu nchini Uingereza ambao Manchester United watakuwa wanatetea kombe lao chini ya kocha mpya David Moyes.
“Nilifikiri kuwasaidia Spurs kucheza UEFA msimu ujao, sijafanikiwa, nawashauri kusajili wachezaji wengine kuimarisha kikosi chao kwa msimu ujao. Ni muhimu sana kumshawishi Bale abaki ili timu iwe bora zaidi”. Alisema Bale.
Boas aliongeza kuwa ni ngumu sana kumuachia mchezaji mwenye uwezo mkubwa kiasi hiki, lazima timu imng`ang`anie kwa nguvu zote.
Tottenham wamemaliza katika nafasi ya tano wakiwa na pointi 72 huku washika bunduki wa London wakimaliza nafasi ya nne kwa kujikusanyia pointi 73, lakini wamekata tiketi ya kucheza ligi ya Uropa msimu ujao.
Bale alifunga bao lake la 26 msimu huu katika mchezo wa jana dhidi ya Sunderland ambapo walishinda bao 1-0 lakini haijawasaidia kufuzu UEFA.
Miamba ya soka la Hispania, Real De Madrid waliomaliza msimu huu bila kikombe, mabingwa wa ligi kuu England, Manchester United na mabingwa wa Bundesliga, wekundu wa kusini mwa Ujerumani, FC Bayern Munich wanahusishwa na mbio kali za kuitaka saini ya nyota huyo.
Msimu wa ligi uliomalizika jana, Bale alishinda tuzo mbili, moja ya mwanasoka bora wa FA na mchezaji bora chipkizi.
Differing faces: Gareth Bale scored another wonder goal against Sunderland, despite showing incredulity at being booked for diving when he felt he was felled in the penalty area (below) 
Gareth Bale alifgunga bao muhimu hapo jana dhidi ya Sunderland na kuipa Spur nafasi ya kucheza ligi ya Uropa msimu ujao
Bale
Confident: Spurs manager Andre Villas-Boas believes Bale will stay at White Hart Lane
KWA KUJIAMINI: Meneja wa Spurs  Andre Villas-Boas anaamini Bale atabaki White Hart Lane
Wakati huo Mwenyekiti wa Spurs  Daniel Levy, ameandika taarifa yake ya mwaka kwa mashabiki na kuchorea majina ya baadhi ya nyota wao anaotamani kuwabakisha akiwemo Bale.
“Msimu huu tunahitaji kuboresha kipindi, tutaendelea kufanya juhudi ya kufanya hivyo na safari hii tunawabakisha wachezaji muhimu kwetu”. Alisema Levy katika taarifa yake.
You must be joking: Spurs felt referee Andre Marriner made costly decisions against their side 
UNATANIA: Wachezaji wa Spurs wakimshangaa mwamuzi wa jana Andre Marriner aliyewanyima penati na kumuonesha kadi ya njano mchezaji Bale kwa madai ya kumdanganya mwamuzi
All smiles: But other results meant Tottenham were consigned to another season in the Europa League 
Walifurahi sana lakini matokeo ya Arsenal yaliwaharibia nafasi yao ya UEFA na sasa watacheza ligi ya Uropa.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video