CHELSEA AMA WAZEE WA DARAJANI SASA WAJIHAKIKISHIA RASMI TIKETI ZA KUCHEZA FAINALI YA UROPA LEAGUE DHIDI YA BENFICA SIKU CHACHE ZIJAZO BAADA YA HAPO JANA KUWACHAPA FC BASEL MAGOLI 3-1 DIMBANI STAMFORD BRIDGE.
FC BASEL ndiyo walikuwa wa kwanza kuifumania nyavu ya mwenzake mnamo dakika ya 45 ya kipindi cha kwanza kupitia mshamuliaji M.Salah, huku magoli ya Chelsea yakifungwa na F.Torres dakika ya 50, Victor Moses dakika ya dakika ya 52 huku Davidi Luiz akisukumiza la tatu na la mwisho mnamo dakika ya 59 ya mchezo.
Nao Benfica jana waliweza kuibuka na ushindi wa magoli 3-1 dhidi ya FC Fenerbahc, ushindi amba utawafanya wakutane uso kwa uso na THE BLUES kwenye fainali.
Goli la kwanza la Benfika lilifungwa na N.Gaitan mapemadakika ya 9, huku nao Fenerbahce wakijibu mashambulizi kwa njia ya penati dakika ya 29 kupitia mshambuliaji D.Kuyt, lakini naye O.Cardozo akiongeza magoli mawili na ya ushindi mnamo dakika ya 35 na 66 ya mchezo kwa upande wa Fenerbahce
0 comments:
Post a Comment