Sunday, May 5, 2013

1
HASSAN BANYAI (KULIA)

Na Baraka Mpenja
Kocha wa zamani wa Temeke Squad na Moro United “Chelsea ya Bongo” Hassan Banyai amesema yupo katika mazungumzo na baadhi ya timu ambazo hakutaka kuzitaja majina ili kupata timu ya kufundisha msimu ujao.
Banyai ambaye alikuwa anaongeza kisomo cha ukocha alisema kuwa kwa sasa anataka kupata timu nzuri ya daraja la kwanza au ligi kuu,  na wakati huu anazungumza na timu nyingi na baada ya kuridhika atatangaza klabu gani ataifundisha.
“Kuwa kocha kuna changamoto nyingi sana, lakini unatakiwa kujipanga vizuri na kujiamini, mwangalie Mourinho licha ya kukabiliwa na changamoto bado anajiamini sana, nafikiri kutumia akili hiyo mara nitakapoanza kazi yangu”. Alisema Banyai.
Kocha huyo aliongeza kuwa akipata timu ya kufundisha atafanya kazi kwa ustadi ili kuendelea kuwajengea imani watanzania kuwa makocha wazawa pia wanaweza kulipatia mafanikio taifa.
Banyai ambaye alikuwa na Moro United msimu wa 2011/2012 alisema bado watanzania hawana imani na makocha wazawa kama wanavyofanya wenzetu hususani Wanigeria ambao walitwaa kombe la mataifa ya Afrika Mwaka huu.
“Ifike wakati na sisi tuige mfano wa mataifa ya magharibi ambao kwa sasa wamejenga imani na makocha wazawa, kama watanzania watawapa sapoti makocha wao tutapata waalimu wazuri ambao wanaweza kufundisha hata nje ya nchi”. Alisema Banyai.
Kocha huyo aliyewahi kufanya kazi na Fred Ferlix Minziro akiwa kocha msaidizi katika kikosi cha Temeke michuano ya Taifa Cup na baadaye kuwa kocha wa timu ya mkoa wa Ilala alisisitiza kuwa hakuna kitu cha maana kama kuwapa nafasi wazawa ingawa hata watu wa nje wana nafasi yake.
“Kwa mfano kama timu ina kocha Mzungu basi wajitahidi kuweka wasaidizi wake wote wawe Watanzania kuliko kuweka wazungu pekee”. Alisema Banyai.
Banyai alisema kasumba ya kutafuta makocha wa nje ipo katika klabu nyingi za Tanzania lakini uwezo wa kifedha ndio kikwazo na kama klabu zingekuwa na uwezo sawa asilimia kubwa zingekuwa na makocha wa kigeni.
“Imebaki kwa timu zetu kubwa Simba, Yanga na Azam ambazo kwa kiasi kikubwa zina uwezo mkubwa wa kifedha, angalia makocha wakuu wote ni wazungu, lakini naamini kuna makocha wa hapa nyumbani ambao wanaweza kufanya kazi nzuri zaidi yao”. Alisisitiza Banyai.
Hakika nabii haheshimiwa kwao, taifa likiiga mfano wa Nigeria, Tanzania itakuwa kitalu cha kuzalisha makocha wenye ubora mkubwa katika mchezo wa mpira wa miguu.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video