Sunday, May 19, 2013

Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
Mshambuliaji hatari wa mabingwa wa soka nchini England, Manchester united, Wayne Rooney hajasafiri na timu yake kuwafuata West Bromwich katika mchezo wa mwisho wa kibabu leo hii kwa makubaliano na kocha wake aliyestaafu kuifundisha United, Alex Ferguson.
Rooney amepewa rukusa ya kubakia kutokana na mke wake Coleen kuwa na uchungu wa kujifunga mtoto wa pili tangu usiku wa jana.
Wawili hao tayari wana mtoto wao wa kwanza mwenye umri wa miaka mitatu anayeita Kai.
Jumapili ya leo (MEI 19)  ndio tamati ya Msimu wa 2012/13 wa BPL, Barclays Premier League, na tayari Bingwa ni Manchester United, Mshindi wa Pili ni Manchester City na Timu 3 zinazoshushwa Daraja ni Wigan, QPR na Reading, lakini bado Timu 2 za nyongeza, kuungana na Man United na City, kwenda kucheza UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI, Msimu ujao hazijapatikana na kimbembe hicho kiko kwa Chelsea, Arsenal na Tottenham.
Hata hivyo, Chelsea wanaonekana wako salama zaidi kwani ni Arsenal tu ndio inaweza kuwapiku kwa Pointi wakati Tottenham wanachoweza kukifanya ni kuifikia Chelsea kwa Pointi lakini kuwapiku ni kitu kigumu maana Chelsea wana Tofauti ya Magoli 35 wakati Tottenham wana 19 tu.
BPL: RATIBA-MECHI ZA MWISHO MSIMU HUU: Chelsea v Everton, Liverpool v QPR, Man City v Nowrich, Newcastle v Arsenal, Southampton v Stoke, Swansea v Fulham,Tottenham v Sunderland, West Brom v Man United, West Ham v Reading, Wigan v Aston Villa
Champion: Wayne Rooney won his fifth title with Manchester United - but will he stay to win another?
UBINGWA: Wayne Rooney msimu huu ameshinda taji la tano akiwa na  Manchester United, je ataweza kushinda lingine?

Hatima yaRooney kubaki OLD TRAFFORD itajulikana siku chache zijazo kufuatia kuwepo kwa taarifa kuwa nyota huyo atakutana na kocha wake mpya David Moyes kujadili suala lake.
Rooney siku za karibuni amekuwa na mawazo kuwa kocha Sir Alex Fergusona amekuwa akimtenga katika kikosi chake na akaomba aruhusiwe kuihama klabu hiyo.
Matumaini ya nyota huyo yamerejea baada ya kocha David Moyes ambaye ni kocha wa zamani wa Everton kuonesha nia ya kutaka kumbakisha united.
Rooney na David Moyes wanatarajiwa kukaa ili kuzungumzia hatima ya Rooney

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video