Thursday, May 2, 2013

TFF Tanzania Prisons

Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe Dar es salaam
Baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 hapo jana dhidi ya JKT Ruvu ya mkoani Pwani uwanja wa Chamazi, maafande wa Tanzania Prisons “wajelajela” hawajasita kuelezea furaha yao na kusema kuwa sasa wapo mikono salama na wanamshukuru Mungu pamoja na wakazi wote wa Mbeya kuwaunga mkono kwa kiasi kikubwa hasa dakika hizi za lala salama.
Katibu mkuu wa Tanzania Prisons Sadick Jumbe ameiambia MATUKIO DUNIANI  kuwa ushindi wa jana umechangiwa na morali kubwa ya wachezaji wao ambao kwa kiasi kikubwa waliahidi kupambana kufa na kupona mbele ya kamati ya saidia Prisons ishinde inayoongozwa na mwenyekiti wake Kamanda wa Polisi Mbeya, Diwani Athman Msuya huku naibu waziri wa elimu na mafunzo ya Ufundi Philipo Mulugo akiwa miongoni mwao.
“Sasa tuna uhakika wa kubakia ligi kuu msimu huu, shukurani kubwa kwa wana Mbeya ambao kwa pamoja wameungana kutuunga mkono na sasa tunawakaribisha wenzetu, klabu ya Mbeya city katika michuano ya ligi hii msimu ujao, sasa mashabiki wa soka wataziona Simba, Yanga, Azam mara mbili kwa msimu mmoja”. Alisema Jumbe.
Katibu huyo wa wajelajela aliongeza kuwa sasa wamebakiza mchezo mmoja nyumbani dhidi ya waliojeruhiwa jana baada ya kufungwa bao moja kwa bila na Polisi Morogoro, nawazungumzia Kagera Sugar, mchezo ambao utakuwa mgumu sana kutokana na Kagera Sugar kujiwekea malengo ya kutwaa nafasi ya pili huku wakipoteza mechi ya jana na kubakia na pointi zao 40.
“Tunajua Kagera ni wagumu sana, harakati za mapambano zinaendelea na haturudi nyuma, mechi ya mwisho hakika hatulazi damu ndugu yangu, tuko na morali kubwa na tunataka kuwaonesha mashabiki wetu kuwa tunatambua mchango wao kwa asilimia zote”. Alisisitiza Jumbe.
Aidha alisema mchezo wa kwanza kule kaitaba walifungwa mabo 2-0, lakini kilichowaathiri ilikuwa ajali mbaya ya gari waliyoipata mzunguko wa kwanza walipokuwa wanaenda mkoani Tanga kupambana na Mgambo,  na baada ya hapo walipumzika kidogo na kutibu wachezajim mwisho wa siku walipoenda kaitaba wakafungwa.
“Kipindi kile tulikwa wagonjwa, sasa tuko sawa, tutapambana kufa na kupona kuhakikisha tunapata matokeo mazuri mechi hiyo ya nyumbani”. Alisema Jumbe.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video