Thursday, May 23, 2013


Benchi la Tanzania Prison linaloongozwa na kocha Jumanne Chale (wakwanza kulia) katika moja ya michezo ya klabu hiyo msimu uliopita (Picha na Maktaba)simbanaprisons5Mashabiki wa Tanzania Prison katika mchezo wa mzunguko wa kwanza wa ligi kuu soka Tanzania bara uwanja wwa Taifa (Picha na maktaba ya Glogalpublisher)

Na Baraka Mpenja 
Wajelajela Tanzania Prisons wameshaanza maandalizi ya kufanya usajili mapema ili kuingia kambini mapema kujiwinda na msimu mpya wa ligi kuu soka Tanzania bara msimu ujao ambapo wamesisitiza kuwa lazima waingie katika kinyang`anyiro cha nafasi tatu za juu kama walivyokuwa wanafanya miaka ya nyuma.
Katibu mkuu wa klabu hiyo Sadick Jumbe, ameimbia MATUKIO DUNIANI kuwa viongozi wameshaona maeneo ambayo yamewasumbua sana katika harakati zao za kukwepa mkasi wa kushuka daraja kuwa ni safu ya kiungo na ushambuliaji.
“Sisi kama viongozi tumekuwa tukifuatilia kwa karibu jinsi timu inavyocheza, tumeona sehemu ya kiungo na ushambuliaji ina matatizo, tunafikiria kuongeza nyota wapya ili kuhimili michuano ya ligi kuu msimu ujao ambao tumehaha kweli kuutafuta”. Alisema Jumbe.
Jumbe alisema kocha mkuu wa klabu hiyo Jumanne Chale bado anaandaa ripoti yake ya ligi ambayo itajumuisha mapendekezo ya wapi kikosi kirekebishwe, lakini viongozi kwa upande wao wameshaona wapi kuna matatizo wakati wanasubiri mwalimu awasilishe ripotu kesho kutwa.
“Chale ambaye tunamuamini sana anamalizia ripoti yake, itatumika akiwa ni muongozo wetu kusajili, lakini tunajua sana wapi kuna matatizo, kwa sababu yeye ni mtaalamu atatusaidia kupata wachezaji watakaotusaidia zaidi”. Alisisitiza Jumbe.
Katibu huyo alisema wamejifunza kitu, mwaka jana walisajili wachezaji ambao hawakuwa na uzoefu, kwa sasa wanataka kutafuta wachezaji wenye uzoefu wa kucheza ligi kuu ili wachanganyikane na wachezaji waliotoka nao ligi daraja la kwanza.
“Unajua wazoefu watasaidia kuongeza nguvu sana, ni muhimu sana kupata wachezaji hao ingawa ni gharama kubwa, lakini halazi mtu damu, lazima tujipange kwa gharama yoyote kupata angalau wachache”. Alisisitiza Jumbe.
Akizungumzia safu ya ulinzi, Jumbe alisema walihangaika kidogo baada ya David Mwantika kutimkia Azam fc, ila haiwapi presha kwani wameshapata mbadala wake ingawa hakumtaja kwa sasa.
“Nadhani watu wanaikumbuka sana Prisons iliyowahi kucheza kombe la shirikisho, sasa inarejea msimu ujao, walitakiwa kutuombe dua mbaya tushuke daraja ili kukwepa cheche zetu, tumefanikiwa kubaki, hakika tunaanza maandalizi mapema mno na lazima tufanye makubwa msimu ujao”. Aliongeza Jumbe.
Pia alisema kubakia ligi kuu msimu huu imekua faraja kubwa kwa mashabiki wa Mbeya waliowapa sapoti kubwa sana hasa kipindi cha mwisho walichokuwa wanachungulia kaburi.
Prisons msimu uliopita imemaliza katika nafasi ya tisa ya msimamo ikijikusanyia pointi 29 kibindoni.
Sasa Mbeya itawakilishwa na timu mbili baada ya Mbeya City kufanikisha kupanda daraja msimu uliopita na kupata nafasi ya kucheza ligi kuu pamoja na Rhino Rangers ya Tabora, na wauza mitumba wa Ashanti United, huku timu za Toto Africans, Africa Lyon na Polisi Morogoro zikiwa zimepisha njia na kutimkia ligi daraja la kwanza.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video