Tuesday, May 21, 2013

Kikosi hiki cha Prisons kimepambana sana msimu huu kubakia ligi kuu soka Tanzania bara baada ya kukabiliwa na changamoto nyingi sana, sasa msimu ujao Mbeya itakuwa na “Mbeya Derby” ambapo mashabiki watakuwa wanazishuhudia timu hasimu za Mbeya City na Tanzania Prisons katika dimba la Sokoine jijini humo 488123_216997305113321_161758080_n 
Hapa ni moja kati ya mazoezi ya Mbeya City chini ya kocha Juma Mwambusi aliyewahi kuifundisha Prisons kwa mafanikioa makubwa, sasa wanaume hao watakabiliana na Prisons msimu ujao

Na Baraka Mpenja
Baada ya kupigana kufa na kupona na hatimaye kufanikisha ndoto zao za kubakia ligi kuu soka Tanzania bara msimu ujao, viongozi wa Klabu ya maafande wa Tanzania Prisons “wajelajela”  wa jijini Mbeya wamekaa kikao cha maandalizi ya kuanza zoezi la usajili ili kuimarisha kikosi chao zaidi.
Katibu mkuu wa wajelajela Sadick Jumbe amiembia MATUKIO DUNIANI kuwa hapo jana walikaa katika kikao cha klabu ili kutathimi hali ya ligi ilivyoenda na wapi kikosi chao kilikuwa na mapungufu makubwa ili kurekebisha.
Jumbe alisema katika kikao hicho wamekubaliana kuongeza wachezaji hasa sehemu ya kiungo ambayo ina shida kubwa sana pamoja na ushambulaiji.
“Tumepigana kufa na kupona, tulijua hatuna uwezo wa kupata nafasi za juu badala yake tulikuwa tunachungulia kaburi, tulipambana na tumefanikiwa kubaki, haya ni mafanikio makubwa sana kwetu na sasa tunajiandaa kufanya usajili mkubwa ili kuimarisha kikosi chetu”. Alisema Jumbe.
Jumbe alipoulizwa ni wachezaji gani wanatarajia kuwasajili, aligoma kuwataja kwa madai kuwa kuna mapapa na dagaa, wao ni dagaa na kama wataanika majina yao basi wanaweza kufanyia umafia na mapapa ambao watawanyang`anya nyota wao.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video