Sunday, May 26, 2013

IMG_5890

Na Baraka Mpenja
Baada ya Simba kutangaza kuwasajili wachezaji watatu kwa mpigo akiwemo mshambuliaji hatari wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Zahor Iddi Pazi aliyekuwa anacheza kwa mkopo JKT Ruvu akitokea Azam fc, Mlinda mlango wa “Wanankulukumbi”  kagera Sugar Andrew Ntala na mlinzi Issa Rashid “Baba ubaya” kutoka Mtibwa sugar, mwenyekiti wa kamati ya usajili ya klabu hiyo Keptein Zacharia Hans Hoppe amesema Simba haina sera ya kuchukua wachezaji kutoka Yanga labda akitokea mzuri, lakini wao wanahangaika kuwachukua wachezaji wa klabu hiyo.
Poppe ameimabia MATUKIO DUNIANI kuwa Simba mwaka huu wanafanya usajili makini tofauti na mwaka jana na ndio maana wameanza kwa kuwaongezea mikataba wachezaji wao, kuwapa vijana wao mikataba na kusajili wapya kama walivyofanya hapo jana.
“Tumewasijili watatu jana, wengi watajiuliza kwanini tumemchukua kipa Ntala, kiukweli hatuna pengo safu ya makipa, tunao wazuri lakini tumeona vyema kuongeza kipa ili apate uzoefu zaidi kwani siku zinaenda”. Alisema Poppe.
Poppe aliongeza kuwa sera yao ya kimya kimya katika usajili bado inaendelea huku akiweka wazi kuwa wanataka kuongeza wachezaji wawili wa kigeni akiwemo beki wa kati na mshambuliaji wa kati ili kuimarisha sehemu hizo ambazo mwalimu amependekeza zitafutiwe nyota wa kuimarisha.
Kuhusu Beki Issa Rashid, Poppe alisema Simba kwa sasa haina beki wa kushoto kwa sasa kwani wanaocheza kwa sasa yaani Haruna Shamte ni beki wa kulia na Paul Ngalema ameomba kusitisha mkataba wake na Simba.
Kuhusu Zahor Pazzi Poppe alisema kwa siku nyingi wamekuwa wakimtaka kwa siku nyingi kwani awali walikuwa na mkataba wa miaka minne naye lakini kuna mambo yalitokea na kufanya wampoteze.


Poppe, ambaye ni Kapteni wa zamani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) alisema wachezaji wote wamesaini mikataba ya miaka miwili kila mmoja.
Poppe amesema Simba SC wanasajili kisayansi na si kama wapinzani wao hao, Yanga SC ambao wanaingia hasara ya fedha nyingi na wanacheza pata potea.
“Sisi tulimsajili Mbuyu Twite kama yeye tu, lakini wao wakaingilia akawapa sharti wamsajili na ndugu yake (Kabange Twite), wakaingia mkenge wakasajili mtu ambaye wamemlipa fedha nyingi, lakini hawajamtumia na hakuwa chaguo lao,”.
Kuhusu suala la Niyonzima, Poppe alisema Yanga wameingizwa mkenge kwa kumlipa dau nono wakiwa na hofu ya Simba kumsajili.
“Niyonzima ni mchezaji wao, sisi hatujawahi kuongea nae kama tunataka kumsajili, nasikia wamempa hela nyingi baada ya kusikia fununu za sisi kumsajili, hatukuonge nae hata kidogo” alisema Poppe.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video