Thursday, May 2, 2013

Na Gervas Mwatebela kwa msaada wa Mtandao
Ni wazi sasa kombe la ligi ya mabingwa barani Ulaya linaelekea Ujerumani baada ya klabu za nchi hiyo kutinga hatua ya fainali,ambapo Bayern Munich imeandika historia kwa kuichapa Barcelona kwa magoli 3 – 0 na kusonga mbele kwa jumla ya magoli 7 – 0  ukijumlisha na magoli 4 – 0.
Magoli ya Bayern Munich yamefungwa na Arjen Robben,goli la kujifunga la beki Gerard Pique na Thomas Mueller yalitosha kuifikisha fainali timu hiyo bingwa wa mara nne wa michuano hiyo kwenda kupambana na ndugu zao Borussia Dortmund ambao waliwaondosha mabingwa wa mara tisa wa michuano hiyo Real Madrid kwa jumla ya magoli 4 – 3.
Barcelona ilitakiwa kushinda magoli 5 – 0  ili kutinga fainali itakayochezwa katika dimba la  Wembley,London Uingereza.Sasa Barca wameungana na ndugu zao Real Madrid ambao licha ya ushindi wa magoli 2 – 0 dhidi ya Borussia Dortmund ya Ujerumani hayakutosha kuwavusha hatua ya fainali.

Kocha Bayern Munich  afichua siri ya ushindi
Kocha  Jupp Heynckes  wa  Bayern Munich amesema siri ya ushindi wa timu yake dhidi ya Barcelona ya Hispania ni kwa sababu vijana wake wana uwezo na wanalijua soka la klabu za Hispania.
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 67 amesema kuwa analifahamu vyema soka la Hispania na falsafa ya klabu ya Barcelona hivyo anawapongeza vijana wake kufuata maelekeza na kuwatupa nje ya michuano klabu ambayo imekuwa tishio kwa takribani miaka nane iliyopita.
‘Nalifahamu soka la kihispaniola,nawajua wachezaji,naifahamu falsafa ya Barcelona,huwa napenda kuangalia mechi za EL CLASSICO yaani Barca ikipambana na Real Madrid huwa naburudika sana.’alisema kocha Jupp.
https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/?ui=2&ik=fadfb7e120&view=att&th=13e65118951c82e9&attid=0.3&disp=inline&realattid=f_hg7v5mz42&safe=1&zw&saduie=AG9B_P8nDams_KBfV7Z-dQcUv9F1&sadet=1367499160986&sads=8vCHOdjP-ct4d0659zcWE8FM-zs
Jupp Heynckes akishangilia ubingwa

Kocha huyo ambaye aliiwezesha Real Madrid kutwaa kombe hilo mwaka 1998 amesema klabu yake inacheza kitimu soka la kasi na lenye malengo ya ushindi ndiyo siri ya mafanikio.
Kocha huyo mbali ya ushindi dhidi Barcelona,pia timu yake ililazimika kuvuka viunzi kadhaa ikiwemo kuitupa nje Arsenal ya England katika hatua ya 16 bora kisha ikawafurusha mashindanoni vinara wa ligi kuu Italia Juventus katika hatua ya Robo fainali.

LIONEL MESSI HAYUKO FITI KABISA-VILANOVA
Kocha wa Barcelona ya Hispania Tito Vilanova amesema  alimuweka nje ya dimba nyota wake Lionel Messi katika mechi ya marejeano dhidi ya Bayern Munich kwa sababu hayuko fiti.
Katika mechi hiyo ya nusu fainali ya pili ambapo Bayern Munich waliwanyanyasa wenyeji wao kwa kuwapiga magoli 3 – 0 hivyo kusonga mbele kwa jumla ya magoli 7 – 0 kwani katika nusu fainali ya kwanza Bavarians walishinda kwa magoli 4 – 0.
Kocha huyo amesema kuwa Messi asingeweza kucheza katika mechi hiyo lakini amekanusha kuwa utegemezi wa BARCA kwa muargentina huyo umesababisha timu hiyo kutolewa katika ligi ya mabingwa barani Ulaya.
Kocha  huyo amesema kuwa Bayern Munich walikuwa bora karibu kila idara kwa mechi zote mbili kuanzia dimbani na kisaikolojia walitimia ndiyo sababu wametinga hatua ya fainali ya ligi ya mabingwa Ulaya.
Kocha huyo amesema kutokuwepo kwa Lionel Messi,Carles Puyol,Eric Abidal na Sergio Busquets siyo kisingizio kwa timu yake kutolewa katika michuano hiyo.
https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/?ui=2&ik=fadfb7e120&view=att&th=13e65118951c82e9&attid=0.1&disp=inline&realattid=f_hg7v30vz1&safe=1&zw&saduie=AG9B_P8nDams_KBfV7Z-dQcUv9F1&sadet=1367498996183&sads=kHDr6QfxAkIEb8checPE-6EuKRY&sadssc=1
TITO VILANOVA

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video