Saturday, May 18, 2013

Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportmail.com
JUMAPILI, MEI 19, ni Siku ya Mwisho ya Msimu 2012/2013 wa ligi kuu soka nchini England “Barclays Premier League”,  na Siku hiyo ndio Mechi ya 1500 kwa Mscotish Sir Alexndar Chapman Ferguson “Kibabu Fergie” akiwa Meneja wa mashetani wekundu, Manchester United na ndio mwisho wa enzi yake kwa vile anastaafu baada ya mechi hiyo.
Sir Alex Ferguson, Miaka 71, amenena: “Ni Mechi ya 15oo, ni mechi yangu ya mwisho, hakika  inashangaza! Nataka kushinda hii kupita ile ya Wiki iliyopita!”
Leo, kwenye Mkutano na Wanahabari kwenye Kambi ya Mazoezi ya Man United huko Carrington ambao ni kawaida ya kila Ijumaa kabla Mechi za Wikiendi, Wanahabari walimpa Sir Alex Ferguson zawadi ya Keki yenye umbo la Mashine ya Kukaushia Nywele ukiwa ni mzaha kuhusu imani ya kwamba Meneja huyo huwapa kibano Wachezaji wake wasipofanya vizuri na kuwafanya wajisikie vichwa vyao moto mithili ya kupitishiwa Mashine hiyo ya Kukaushia Nywele.
Akijibu kwa mzaha, Ferguson alisema: “Inastahili! Kuna wakati sikukubaliana nanyi na kile kilichoandikwa na kuna wakati mliandika vitu vizuri tu na nilividharau. Lakini Siku zote sikuweka kinyongo wala kisasi. Hiyo si staili yangu!”
Ferguson pia alithibitisha kuwa Kipa Anders Lindegaard atakaa Golini Mechi na WBA na Masentahafu watakuwa Jonny Evans na Phil Jones huku Nemanja Vidic na Rio Ferdinand wakiwa Benchi akisisitiza sasa ni zama za Vijana
Jumapili iliyopita Sir Alex Ferguson aliagwa kwa shangwe walipocheza Mechi na Swansea City Uwanjani Old Trafford, ikiwa ni Mechi yake ya mwisho Uwanjani hapo, na kushinda Bao 2-1 na Jumatatu Timu nzima ya Man United ilitembeza Kombe la Ubingwa wa BPL kwenye Mitaa ya Manchester na kusindikizwa na Maelfu ya Washabiki hadi katikati ya Jiji, eneo la Albert Square, walipopokewa na Maelfu ya Umati.
Mwenyewe Ferguson amekiri kuwa mapokezi ya Wiki iliyopita yalishinda yale ya Mwaka 1999 walipopita Mitaani baada ya kutwaa Trebo, yaani Ubingwa wa England, FA CUP na UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI, na kuweka Historia ya kuwa Klabu ya kwanza na pekee Uingereza kufanya hilo.
Happy retirement: Fergie seemed in a jovial mood during the press conferenceANASTAAFU AKIWA NA FURAHA KUBWA: Fergie ameonekana mwenye furaha kubwa sana leo katika mkutano wake wa mwisho na wanahabari
Ferguson
Bowing out: Ferguson leaves Manchester United after 27 years at the top 
Daah! si mchezo: Ferguson anastaafu kuifundisha United baada ya kukaa na timu kwa miaka 27 akiwa kocha mkuu
Presence: Ferguson still held the power in the press conference, but looked more relaxed than usualrelaxed
Kibabu akifurahia tu, hana shida kwa sasa
Incredible: Ferguson was thrilled by the crowds that turned out on Monday 
Ferguson aliwaongoza wachezaji wake kupita mitaa mbalimbali ya jijini Manchester kushangilia ubingwa wake wa 20 jumatatu ya wiki hii
Back in the day: United's Treble-winning squad on their 1999 victory parade 
MIAKA YA NYUMA: Huu ni ubingwa wa United wa mwaka  1999 ambao Fegie alitwaa  
Presence: Ferguson still held the power in the press conference, but looked more relaxed than usualrelaxed  
Kipato huleta majivuno, nini cha kumnyima raha kibabu?, kafanikiwa kila kona akiwa na United
18 May 2013

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video