Wednesday, May 22, 2013

stars 07

Na Baraka Mpenja
Mwamuzi atakayeshika kipenga katika mchezo wa kuwania kufuzu fainali za kombe la dunia mwakani nchini Brazil kati ya timu ya taifa ya Tanzania “Taifa Stars” dhidi ya Simba wa milima ya Atlas, timu ya taifa ya Morroco amewekwa hadharani.
Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limemteua mwamuzi kutoka Afrika Kusini anayejulikana kwa jina la Fraser Daniel Bennett.
 Mechi hiyo ya kundi C itapigwa juni 8 mwaka huu jijini Marrakech, Morocco kwenye Uwanja wa Grand kuanzia saa 3 kamili usiku kwa saa za Morocco.
Bennett atasaidiwa na Thusi Zakhele Siwela pia wa Afrika Kusini, wakati mwamuzi msaidizi namba mbili atakuwa ni Marwa Range kutoka Kenya. Mwamuzi wa akiba (fourth official) ni Lwandile Mfiki wa Afrika Kusini.
 Kamishna wa mechi hiyo ni Robert Mangollo-M’voulou wa Gabon wakati mtathimini wa waamuzi (referee assessor) ni Charles Masembe kutoka Uganda.
 Taifa Stars ambayo iko chini ya Kocha Kim Poulsen, na ikidhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager tayari iko kambini katika hoteli ya Tansoma ikiendelea kujinoa kwa ajili ya mechi hiyo ambapo kabla itajipima na Sudan (Nile Crocodiles) Juni 2 mwaka huu jijini Addis Ababa, Ethiopia.
 Ratiba ya mazoezi kwa timu hiyo ni kama ifuatavyo;
Mei 22                 Saa 10 jioni                             Uwanja wa Karume
Mei 23                 Saa 1 asubuhi na Saa 10 jioni   Uwanja wa Karume
Mei 23                 Saa 10 jioni                             Uwanja wa Karume
  Mei 25                 Saa 1 asubuhi na Saa 10 jioni     Uwanja wa Karume
Mei 26                 Saa 3 asubuhi                            Uwanja wa Karume
 Katika mchezo wa kwanza uliopigwa uwanja wa taifa jijini Dar es salaam, Taifa stars iliifunga Morroco mabao 3-1 huku mabao mawili yakitiwa kimiani na Mtanzania Mbwana Samata anayekipiga TP Mazembe ya DRC Kongo na bao moja likifungwa na Thomas Ulimwengu wa TP Mazembe.
Kabla ya mechi hiyo, kocha wa stars Mdenimark Kim Paulsen alisafiri kwenda nchini Afrika kusini kuona mechi za kombe la mataifa ya Afrika ambapo Morroco na Ivory Coast, wapinzani wa stars walishiriki na mwalimu kuwasoma vizuri sana.
Stars wakitoka Morroco watacheza na Ivory Coast uwanja wa taifa jijini Dar es salaam wakihitaji kufuta kipigo cha mabao 2-0 walichoambulia jijini Abijan nchini Ivory coast mwaka jana.
Baada ya kumaliza kipute hicho Stars itawafuata Gambia nyumbani kwao huku ikiwa na kumbukumbu ya kuwatungua mabao 2-1 uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.
Stars ipo kundi C na mpaka sasa ipo nafasi ya pili ikiwa na pointi 6 nyuma ya Ivory Coast wenye pointi 7 kibindoni.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video