Sunday, May 19, 2013


Wachezaji wa Yanga wakishangilia baada ya kupata goli la kwanza dhidi ya Simba. Bao hilo lilifunga dakika ya tano ya kipindi cha kwanza baada ya mabeki wa Simba kufanya makosa makubwa langoni mwao_MG_0386 
Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe Dar es salaam
Kocha wa klabu mpya ya ligi kuu soka Tanzania bara msimu ujao, Mbeya City kutoka jijini Mbeya, Mwalimu Juma Mwambusi amesema kilichowagharimu wekundu wa Msimbazi Simba katika kipute cha watani wa jadi na kufungwa mabao 2-0 ni nafasi ya ulinzi kupwaya kwa msimu mzima wa ligi hiyo.
Mwambusi ameimabia MATUKIO DUNIANI kuwa makocha wa Simba wamehangaika sana kutafuta wachezaji wa kucheza nafasi ya ulinzi ili kuziba pengo la baadhi ya wachezaji waliotimka Msimbazi akiwemo beki wa kati wa Yanga Kelvin Patrick Philip Yondan aliyeihama Simba mwishoni mwa msimu wa mwaka jana.
Kocha huyo aliyekuwepo uwanja wa taifa hapo jana kushuhudia mtanange huo uliovuta hisia za mashabiki wengi nchini Tanzania amesisitiza kuwa bao la kwanza la Yanga lilifungwa baada ya mabeki wa Simba kushindwa kukaba vizuri na kujua wapi mpira utatua.
“Kipa Juma Kaseja aliwapanga mabeki wake upande wa kulia kwake na mpira ulitua kule, lakini akasahau upande wa kushoto ambao angekaa yeye, angalia Kavumbagu alivyopiga kichwa chepesi na kuingia katika kona ya goli ambapo hakukuwa na mlinzi yeyote, lile ni kosa kubwa”. Alisema Mwambusi.
Mwambusi aliyesisitiza kuwa jana alilazimika kufika uwanjani ili kujifunza zaidi kuliko kutazama mpira kama shabiki wa kawaida aliongeza kuwa hata bao la pili la Hamis Kiiza lilitiwa kambani kufuatia uzembe wa mabeki wa Simba kushindwa kuosha mpira wa kona langoni kwao.
“Sisi walimu huwa tunawafundisha wachezaji kuwa lazima beki aangalie mpira utatua wapi na jinsi wachezaji wa timu pinzani alivyokaa  (watch the ball, watch the opponent players movement) , wakati kona inapigwa mabeki wa Simba hawakuangalia wachezaji wa Yanga wamekaa vipi na hatari iko wapi, mpira ulimkuta sehemu nzuri Kiiza na kufunga bao rahisi”. Alisema kitaalamu Mwambusi.
Kocha huyo aliendelea kueleza kuwa walinzi wa Simba wanaocheza nafasi hiyo kiukweli asili yao siyo mabeki.
“Muangalie Kapombe ambaye ni kiraka, anachezeshwa sehemu ya beki wa kati wakati yeye anafanya vizuri zaidi pembeni, hata Musa Mude ni kiungo, lakini mwalimu kalazimika kumchezesha nafasi ya ulinzi, ukiwaangalia mara nyingi wanakosa mawasiliano mazuri na ndio maana jana wamepoteana sana”. Alisema Mwambusi.
Akizungumzia kikosi cha Simba, Mwambusi alisema watu wengi waliibeza klabu hiyo, lakini yeye ameona kuwa Simba ina wachezaji bomba ambao kama watatunzwa msimu ujao wa ligi watakuwa na timu bora zaidi.
“Wachezaji vijana wamefanya kazi nzuri sana na wanaonekana kuwa makini na kutulia sana, wakiendelea kuwa pamoja na kucheza kwa muda mrefu, Simba itakuwa tishio”. Alisema Mwambusi.
Mwambusi alisema Simba kwa sasa bado ina matatizo na haijatengamaa ukilingaisha na msimu uliopita, na hii inatokana na kushindwa kupata wachezaji mbadala wa baadhi ya nyota wake waliotimka.
“Pengo la Yondan bado lipo, Emmanuel Okwi, ma Marehemu Patrick Mafisango, hakika kukosekana kwa wachezaji hawa imekuwa tatizo kubwa kwa Simba, nadhani timu ipo wakati wa mpito na itawahitaji kutulia na kutengeneza kikosi chake”.
Pia alisema mechi ya jana imempa nafasi ya kujua falsafa za Soka la Simba na Yanga hata kama wanaweza kubabili, hivyo inampa changamoto ya nini cha kufanya akiwa na kikosi chake cha Mbeya City msimu ujao.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video