Monday, May 20, 2013

Y

Na Baraka Mpenja
Viongozi wa mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2012/2013, “Kwalalumpa Malysia” Dar Young Africans wamesema wanaandaa utaratibu maalumu wa kusherehekea ubingwa wao wa 24 na wanachama wao.
Katibu mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako ameimbia MATUKIO DUNIANI  kuwa sherehe zimeanza tangu juzi, lakini wanajipanga kuaandaa siku maalumu kushangiliwa ubingwa wao.
“Watu hawakulala hata kidogo baada ya kuwafunga Simba, sherehe zile hazitoshi, sasa tunaandaa sherehe ya pamoja kufurahi kwa pamoja na mashabiki wetu”. Alisema Mwalusako.
Mwalusako aliongeza kuwa viongozi wa Yanga wamefurahi sana kutwaa ubingwa kabla ya ligi kumalizika na kuwatandika watani zao wa jadi mabao 2-0 katika mechi ya kufunga pazia la ligi kuu msimu huu.
“Waliongea sana na wakajitapa, mimi nilisema wakati wa meneno umekwisha, tusubiri siku ya mechi, kweli siku ikafika tukawafunga, ni raha sana kwetu”. Alisema Mwalusako.
Katibu huyo alisisitiza kuwa ubingwa wa msimu huu umetokana na sababu nyingi sana , lakini kubwa zaidi ni ushirikiano mkubwa wa viongozi, mashabiki na wanachama wa Yanga.
“Viongozi tumefurahishwa sana na umoja wa mashabiki wetu, angalia uwanja ulivyofurika mashabiki wa rangi ya kijani na njano, tunawashukuru sana”. Alisema Mwalusako.
Mwalusako aliongeza kuwa ubingwa wa msimu huu ndio mwanzo wa mapambano, sasa wanajipanga kwa ajili ya mashindano ya kimataifa na lazima wafanye vizuri.
Akiwazungumzia wapinzani wao Simba, Mwalusako alisemanwana timu nzuri na wanacheza vizuri sana.
“Wako vizuri, lakini hawana ubora zaidi yetu, sisi ni wazuri sana, nafikiri baada ya miaka mitano ijayo watatufikia kuwa na kikosi bora”. Alisema Mwalusako.
Wakati Mwalusako akitamba, naye katibu mkuu wa baraza la wazee wa Yanga, Ibrahim Akilimali alisema leo hii wanakutana pamoja kufurahi baada ya kuwafunga Simba.
“Nilisema lazima mnyama achinjwe, na amechinjwa kwa risasi mbili tu. Alitufunga tano kwasababu wazee tulivua kofia na safari hii hatukuvua kofia, matokeo yake wamepigwa kama kawaida, leo tunakutana kufurahi pamoja”. Alisema Akilimali.
Baada ya kutwaa ubingwa, sasa Yanga wataliwakilisha taifa katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika ambayo wenzao Simba walitolewa kwa kufungwa nje ndani na Libolo ya Angola.
Walifungwa bao moja sifuri uwanja wa taifa na wakatandikwa mabao 4-0 nchini Angola.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video