Friday, May 17, 2013

181066_568992019785435_478320816_n
Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe Dar es salaam
KITABU cha kwanza nchini kinachozungumzia soka la Tanzania kijulikanacho kwa jina la “Soka la Tanzania” kitaanza kuuzwa leo katika maeneo tofauti ya jiji la Dar es salaam, lakini siku ya kesho kwenye mechi ya watani wa Jadi, Yanga na Simba kitauzwa kwa wingi zaidi.
 Akizungumza na MATUKIO DUNIANI, mtunzi wa kitabu hicho, Katibu Mkuu wa zamani wa Shirikisho la Kandanda nchini (TFF), na mdau mkubwa wa kandanda Fredrick Mwakalebela amesema kitabu hicho gharama yake ni shilingi elfu kumi tu (10,000) na tayari kila kitu kinakwenda sawa.
Mwakalebela alisema kuwa kwa sasa ametoa nakala 10,000 kwa ajili ya kuuzwa Tanzania nzima.
Alisisitiza kuwa kitabu hiki ni muhimu sana kwa wana-habari, wachezaji, makocha, waamuzi na wadau wengine wa mchezo huo kwani kuna kumbukumbu zote za mechi za timu ya Taifa ikiwa mabao ya kufunga, wafungaji, vikosi tofauti vya timu za taifa na mambo mengine.
“Nakala hizo ni mwanzo tu, nafikiri nitatoa nyingi zaidi ili ziwafikie watanzania. Hata kwa waandishi wa habari ni muhimu sana kwani kinaweza kutumiwa kama mrejeo wa matukio mbalimbali ya soka letu”. Alisema Mwakalebela.
Katibu huyo wa zamani wa TFF na mdau wa soka la Tanzania aliongeza kuwa kitabu hicho kimezungumzia historia ya soka la Tanzania katika Nyanja za vijana, wanawake na wanaume, ligi kuu ya Tanzania Bara, Taifa Cup, Timu ya Taifa na Utawala Bora.
“Ni kitabu kizuri sana, hutapoteza pesa yako, kitakupa taarifa nyingi sana pamoja na kumbukumbu za soka letu, vikosi vya zamani, kauli za makocha waliopita na mstakabali wa soka letu”. Alisema Mwakalebela.
Mbali ya hayo, kitabu hicho kimezungumzia ujio wa kocha Marcio Maximo, mchango wa serikali katika kuinua mpira wa miguu, wadhamini, uhusiano kati ya waandishi wa habari na TFF na changamoto mbali mbali za mpira wa miguu Tanzania.
“Pia nimeelezea mambo niliyojifunza chini ya Rais Leodegar Tenga kwa kipindi cha miaka mine nikiwa TFF, matatizo niliyokutana nayo kutoka kwa makamandoo na kuniita mimi muimba kwaya wakati wa utambulisho wangu wa kwanza  Juni 15, 2006,” alisema Mwakalebela.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video