Na Baraka Mpenja kwa Msaada wa Sportsmail.com
Baada
ya kusambaa kwa taarifa za kocha wa Real Madrid Mario Jose Dos Santos
Mourinho katika vyombo vya habari kuwa anataka kurudi klabu yake ya
zamani, Chelsea ya London, leo hii kocha huyo amesema mpaka sasa
hajafanya maamuzi wapi anaelekea baada ya kufikiria kuachana na klabu
yake ya sasa.
Mourinho
baada ya jumanne ya wiki hii kutolewa na Borussia Dortmund ligi ya
mabingwa barani ulaya alisema kuwa kwa sasa anataka kurudi Uingereza na
anapenda ligi ya huko tofauti na Uhispania.
Kocha
huyo mwenye maneno mengi katika mkutano na waandishi wa habari leo hii
kuelekea katika mchezo wa kesho dhidi ya Real Valladolid hajasema lolote
mbali na kuzungumzia mchezo huo.
Mourinho alisema “Haina maana kuongelea hilo kwa sasa kama naenda ama la, kama naenda sitahitaji kutoa maelezo”
Aliongeza kuwa yeye ni kocha mtaalamu na bado anaiheshimu klabu yake ya sasa lakini akimaliza ligi atazungumza wapi anakwenda.
“Sijachukua maamuzi mpaka sasa, kwanza mkumbuke kuwa mke wangu na wanangu ndio wanajua mimi naenda wapi”. alisistiza Mourinho.
Kocha
alisisitiza kuwa ataongeza zaidi baada ya ligi kuisha kwani bado ana
mechi kadhaa, pia anacheza fainali ya kombe la Copa del Rey.
SIJAAMUA BADO: Jose Mourinho alisisitiza sijachukua maamuzi mpaka sasa kuhusu maisha yangu ya baadaye
SIRI KUBWA: Mourinho Alisema familia yake ndio wanajua wapi anaenda
TAARIFA ZA CHINI CHINI: Mourinho anajipanga kurudi Chelsea.
0 comments:
Post a Comment