Saturday, May 4, 2013

6
Mrisho Khalfan Ngasa (kushoto) akionesha ufundi wa kumiliki gozi la ng`ombe mbele ya mchezaji wa Ruvu Shooting mechi za nyuma

Na Baraka Mpenja
Mnyama pori, Simba ya Dar es salaam kesho ndio kesho, wanashuka ugani kuburuzana na maafande wa Ruvu Shooting katika mchezo wa ligi kuu soka Tanzania bara uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Mchezo wa kesho unatokana na mechi baina ya timu hizo iliyotakiwa kuchezwa aprili 25 kuahirishwa kwa kile kilichoadaiwa kuwa uwanja wa taifa ulikuwa katika matumizi ya sherehe za Muungano aprili 26 mwaka huu.
Taarifa za kuahirishwa kwa mechi hiyo zilikuja kwa ghafla sana na kuwashangaza mashabiki wengi wa soka kwani taarifa ilitolewa siku ya mechi na shiriksiho la soka Tanzania TFF.
Timu zote zilieleza masikitiko yao kuhusu kuahirishwa ghafla mechi hiyo kufuatia kukamilisha maandalizi ya mechi hiyo, lakini siku ndio inawadia ambayo ni kesho uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.
Kuelekea katika kipute hicho timu zote zimetamba kuibuka na ushindi, huku tambo za mashabiki zikiendelea kila kona ya jiji.
Kocha msaidizi wa Simba, Jamhuri Kiwhelu “Julio Alberto” ameimabia MATUKIO DUNIANI kuwa maandalizi ya mechi yamekamilika na kikosi chao kipo salama chini ya kocha mkuu Mfaransa Patrick Liewig.
Julio alisema kikosi cha Mnyama ambacho kimesheheni makinda wengi kitacheza soka la kitabuni na kuwafurahisha mashabiki wao watakaofurika uwanja wa taifa.
“Sisi tunajenga kikosi na tunajua kwamba muda unahitajika, tunamshukuru Mungu kwa kutupa uzima na kesho tutacheza kutafuta ushindi mnono mbele ya Shooting ambao ni timu nzuri”.
Julio aliongeza kuwa siku zote ukitaka kuona raha ya soka ukutane na Ruvu Shooting ya Mkwasa kwani wanacheza soka safi na hapo kesho watakutana wataalamu wa soka na kutoa burudani maridhawa.
Wakati Julio akitamba kuwafunga Shooting, maafande hao kupitia kwa afisa habari wake Masau Bwire wamesema kuwa kauli ya Simba kuwa wanataka kulinda heshima yao kesho itagonga mwamba kwani watachinjwa tu.
Masau alisisitiza kuwa wamejiandaa kwa uzuri sana na wanajua Simba wana machungu ya kupoteza ubingwa na kuelekea kukosa nafasi ya pili, lakini wamejipanga kupambana nao kupunguza machungu ya kushindwa kuwafunga Oljoro mchezo wa nyumbani wiki iliyopita.
“Simba sio timu ya kutubabaisha, wanajua soka la Ruvu shooting, mashabiki wasikose taifa kesho, hakika kutakuwa na burudani kubwa sana, tuko fiti sana kupambana na mnyama”. Alitamba Masau.
Simba wanaingia katika mchezo wa kesho wakiwa nafasi ya nne ya msimamo wakijikusanyia pointi 39 na Ruvu Shooting wanaofundishwa na Charles Boniface Mkwasa wapo nafasi ya saba wakiwa na pointi 31 kibindoni.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video