Tuesday, May 21, 2013

Beki wa Yanga anayevalia jezi nambari tatu, Stephano Mwasyika (kushoto) akimiliki gozi la ng`ombe katika moja ya mechi alizoichezea Yanga  shangilia 
Stephano Mwasyika (kushoto), Hamis Kiiza Diego (katikati) na Said Bahanuz (kulia) wakishangilia moja la bao ambalo Yanga ilifunga mechi za Nyuma

Na Baraka Mpenja 
 
Baada ya msimu wa ligi kuu kumalizika mei 18, habari ya mjini kwa sasa ni vuguvugu la usajili, timu zimeanza kutunishiana misuli. Jana Yanga wameanza kwa kumsajili Mrisho Ngassa.
Mtandao huu unaendelea kufanya jitihada za kuwatafuta wachezaji mbalimbali ili kuzungumza nao juu ya maisha yao ya baadaye na hali ya ligi ilivyokuwa.
Tumeanza na wachezaji wa Yanga ambao wametwaa ubingwa, tuliongea na Frank Domayo, Nadir Haroub “Canavaro” na leo hii tumekutana na beki wa kushoto wa Yanga, Stephano Mwasyika. Fuatilia mahojiano na nyota huyo aliyekaa benchi kwa muda mrefu msimu huu;
MATUKIO DUNIANI: Stephano Mwasyika habari yako?
MWASYIKA: Safi! Habari ya kazi ndugu yangu?
MATUKIO DUNIANI: Salama
MWASYIKA: Nambie kaka?
MATUKIO DUNIANI: Hongera kwa kumaliza msimu wa ligi kuu soka Tanzania bara salama salimini!
MWASYIKA: Asante sana,  tunamshukuru Mungu
MATUKIO DUNIANI: Ubingwa wa mwaka huu ni wa pili kwako ukiwa na Yanga, unajisikiaje kwa mafanikio hayo?
MWASYIKA: Daah! Nimefurahi sana kaka! Unajua mimi kama mchezaji siku zote naota mafanikio, na baada ya kutwaa ubingwa mwaka huu huku tukiwafunga Simba mabao 2-0, ni faraja kwangu na famila yangu pia.
MATUKIO DUNIANI: Vipi mbona umesugua benchi sana msimu, uwezo wako umeshuka?
MWASYIKA: Hapana! Bado mimi nina uwezo mkubwa sana, nafanya mazoezi na timu,  kila kitu kipo sawa. Kwanini sipangwi hiyo ni ishu nyingine, kuna sababu binafsi ambazo siwezi kusema kwa sasa, lakini kuna mipango nafanya,  nikiweka sawa nitakutaarifu tupige stori vizuri, kwasasa liache kaka!.
MATUKIO DUNIANI: Kwanini huwezi kusema?
MWASYIKA: Usiwe na shaka, nitakuambia tu, lakini kwa sasa liache kwanza, nikiweka mambo sawa nitakuita nikupe mpango.
MATUKIO DUNIANI: Licha ya kutokucheza msimu huu, unakionaje kikosi cha Yanga?
MWASYIKA: Nafikiri kikosi ni kizuri, wachezaji wana uwezo mkubwa sana, kila mmoja anajitahidi kutafuta nafasi ya kucheza. Ushindani ni mkubwa sana, nafikiri timu itafanya vizuri sana michuano ya kimataifa.
MATUKIO DUNIANI: Yanga jana imemnasa Ngassa, unaonaje urejeo wa nyota huyo?
MWASYIKA: “That is good” ni bonge la mchezaji, namkubali sana. Ujio wake ni sahihi na amerudi timu yake sahihi. Karibu sana Ngassa.
MATUKIO DUNIANI: Vipi kuhusu wewe, utasaini Yanga?
MWASYIKA: Ni mapema sana, nafikiri kuna mambo nayafanya kama nilivyokuambia awali, ikifika muda wake nitakuambia wala usijali.
MATUKIO DUNIANI: Kwanini unaweka siri, kwani ni dhambi?
MWASYIKA: Nitakuambia bwana, subiri nijiweke sawa.
MATUKIO DUNIANI: Vipi ushindani wa ligi kuu msimu huu?
MWASYIKA: Ushindani ulikuwa mkubwa sana na kuna timu ambazo zimecheza vizuri sana. Mimi nimeshuhudia timu zote, lakini timu ya Boniface Mkwasa, Ruvu Shooting nafikiri imecheza kitimu zaidi na inajua kucheza, sema tatizo ni kukosa kujiamini katika michezo yake. Pia Simba, Azam fc, Kagera, Coastal Union zimecheza soka zuri sana na zinastahili sana kuwepo ligi kuu Tanzania bara.
MATUKIO DUNIANI: Siku zijazo timu hizi zinaweza kuondoa ufalme wa Simba na Yanga?
MATUKIO DUNIANI: Daaah! Siwezi kulisemea hilo, soka ni mipango, kama watawekeza vizuri wanaweza kufanya vizuri na kuleta changamoto kwa timu za simba na Yanga. Angalia Azam wanavyojitahidi sasa.
MATUKIO DUNIANI: Ligi umemalizika, unapumzika wapi safari hii?
MWASYIKA: Baada ya siku nne zijazo nataka kwenda nyumbani mkoani Mbeya kuwasalimia wazazi. Kwa sasa nipo zangu geto maeneo ya Ilala. Karibu sana.
MATUKIO DUNIANI: Asante Mwasyika, nitafika huko tupige stori, kumbuka umesema kuna mambo unayafuatilia halafu utatuambia!.
MWASYIKA: Tuko pamoja wala usijali, nitakuambia.
Mpenzi msomaji wa mtandao huu, haya ni mazungumzo na beki wa kushoto wa klabu ya Yanga, Stephano Mwasyika.
Alisema kuna mambo anayafanya juu ya mkataba, muda si mrefu atatujuza wapi anaelekea, je, Atabaki Yanga au anaihama klabu hiyo?. Tusubiri.
Endelea kufuatilia habari hii hapa hapa MATUKIO DUNIANI.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video