Thursday, May 23, 2013


Kocha Charles Boniface Mkwasa akiwa katika kazi yake michezo ya nyuma (picha na maktaba)ruvu shooting 
Kikosi cha Ruvu Shooting katika moja ya mechi za ligi kuu soka Tanzania bara msimu uliopita

Na Baraka Mpenja
Miongoni mwa klabu zinazotajwa kutandaza soka la kisasa, kucheza kwa ushirikiano katika idara zote kwa maana ya ngome ya ulinzi, dimba la kati na mhimili wa kupachika mabao kimiani safu ya ushumbuliaji ni maafande wa jeshi la kujenga taifa wa mkoani Pwani Ruvu Shooting.
 Wakati makocha mbalimbali wa soka, wachezaji, mashabiki na wadau wakikimwagia sifa za kumwaga kikosi cha wapiga kwata hao kutoka Pwani, kocha mkuu wa klabu hiyo, Charles  Boniface Mkwasa “Master” ameimbia MATUKIO DUNIANI kuwa anafurahi sana kupongezwa na wapenzi wa soka kuwa kikosi chake kimecheza soka safi msimu uliomalizika mei 18 ingawa ameanika madhaifu ya kikosi hicho kuwa safu ya ushambuliaji haina makali ya kunyoa timu pinzani.
Mkwasa alisema mara nyingi wachezaji wake walipata nafasi nyingi sana katika mechi tofauti, lakini walikuwa wanazichezea sana na kuinyima klabu hiyo ushindi muhimu ambao ungewafanya washike nafasi nzuri zaidi.
“Kwa ujumla vijana walicheza vizuri sana ingawa mechi nyingi hatukushinda, bahati mbaya sana timu imekosa nafasi nzuri, lakini tungekuwa makini katika nafasi ya ushambuliaji tungefika mbali zaidi msimu uliomalizika wiki iliyopita”. Alisema Mkwasa.
Kocha huyo aliongeza kuwa mara zote amekuwa akiwataka wachezaji wake kucheza kitimu na kuachana na tabia ya kucheza kibinafsi kwani soka hilo limepitwa na wakati.
“Zamani kupiga chenga ilikuwa sifa sana, siku hizi soka linachezwa kitimu, sikatai kutumia uwezo binafsi pale inapobidi, lakini kucheza kitimu inasaidia timu kufanya vizuri, mimi ni mwalimu, nafundisha soka la kitimu zaidi, vijanabwamekuwa wakinielewa vizuri sana”. Alisema Mkwasa.
Mkwasa pia amewatupia lawama baadhi ya waamuzi waliokuwa wanachezesha mitanange ya ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2013/2013 kuwa wameboronga sana hivyo kuwaathiri sana katika michezo yao.
Kocha huyo aliyewahi kuwa kocha wa timu ya taifa ya wanawake Twigar stars alishauri waamuzi kujirekebishe sana msimu ujao ili kutojenga mazingira ya kukosewa imani.
“Kuna mambo ambayo waamuzi wameyafanya mpaka aibu, kila mtu alikuwa anashangaa uwanjani kwa kile kinachotokea, lakini waamuzi huwa wana mamlaka makubwa sana uwanjani, ndio maana tunakaa kimya, binafsi nawaaomba wabadilke na kamati ya kutathmini waamuzi iliangalia hilo kwa kina”.
Kujiandaa na msimu ujao Mkwasa alisema kuwa lazima aongeze washambuliaji wa kuongeza makali zaidi msimu ujao.
Mkwasa alisema akipata washambuliaji wazuri wa kati na mawinga atakufa na mtu msimu ujao na kuingia tatu bora ni lazima.
Msimu wa ligi kuu uliomaliza mei 18 mwaka huu, Ruvu shooting walikipiga na Toto Africans ya Mwanza walioshuka daraja na kuambulia kipigo cha mabao 2-0 na kufikisha pointi 32 katika nafasi ya saba.
Mkwasa alisisitiza kuwa kumaliza nafasi ya saba haijampa faraja hata kidogo kwani hesabu zake zilikuwa kukaa nafasi tatu za juu.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video