Sunday, May 19, 2013

TFF Mgambo JKT

Na Baraka Mpenja
Shangwe, nderemo na vifijo vimetawala miongoni mwa mashabiki wa kandanda katika jiji la Tanga baada ya klabu ya maafande wa Mgambo JKT kufanikiwa kubakia ligi kuu  msimu ujao.
Katibu mkuu wa klabu hiyo Antony Mgaya ameimbai MATUKIO DUNIANI kuwa ushindi wa jana wa bao 1-0 katika uwanja wao wa nyumbani wa CCM Mkwakwani Mkoani Tanga umewapa furaha kubwa baada ya kuumiza vichwa vyao kwa muda mrefu wakihitaji kutafuta njia ya kubakia ligi kuu.
“Ilikuwa ngumu sana kwetu, ushindani ulikuwa mkubwa, kuna wakati tukakosa matumaini baada ya kufungwa kila mchezo muhimu kwetu, lakini tukaendelea kujipa moyo na hatimaye tumefanikiwa”. Alisema Mgaya.
Mgaya aliyeonekana kuikubali imani ya dini kuwa Menyezi Mungu amewaona na kuwasaidia alisema Mungu amesikia kilio chao wakati wa vita ya kukwepa mkasi wa kushuka daraja .
“Kila mtu alikuwa anamuomba mungu ili anusurike, lakini katusaidia sisi kwa kutupa nguvu ya kupambana mpaka mwisho”. Mgaya Alisema kwa furaha kubwa.
Kiongozi huyo alisisitiza kuwa mafanikio hayo si yao pekee, bali ni ya Mkoa mzima kwani mashabiki, viongozi na wadau wa soka waliwaunga mkono sana mpaka mwisho wa ligi.
Mgaya alisema sasa wamemaliza ligi salama na wanamsubiri kocha wao Mohamed Kampira aandike ripoti yake itakayojumuisha mapendekezo ya usajili , na viongozi wapo tayari kuanza shughuli ya kutafuta wachezaji wapya.
“Ulikuwa msimu wa kwanza kwetu, tumejifunza mengi sana, lazima tusajili wachezaji wengine ili kuendana na ushindani wa ligi hii msimu unaokuja”. Alisema Mgaya.
Timu zilizoshuka daraja ni tatu ambazo ni wana kishamapanda Toto Africans, Polisi Morogor na Africa Lyon.
Na timu mpya ni tatu ambazo ni Mbeya City ya Mbeya, Maafande wa Rhino Rangers kutoka Tabora na wauza Mitumba wa Ashant United kutoka jijini Dar es salaam.
Msimu mpya wa ligi kuu unatarajia kuanza kati ya mwizi Agosti na Septemba maka huu.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video