Saturday, May 4, 2013

1
Mecky Mexime akifuatilia moja ya mechi ya ligi kuu soka Tanzania bara wakati timu yake ipo dimbani

Na Baraka Mpenja
Nahodha na mlinzi wa kushoto wa zamani wa timu ya taifa ya Tanzania “Taifa stars” na sasa kocha mkuu wa klabu ya soka ya Mtibwa sugar “wana TamTam” na mchezaji wa zamani wa klabu hiyo, Mecky Mexeme amekiri kuwa msimu huu wa ligi kuu soka Tanzania bara umekuwa mgumu zaidi kutokana na uwezo mkubwa wa kila timu shiriki.
Mexime ameimbia MATUKIO DUNIANI kuwa unaweza kujipanga kupata ushindi katika mchezo fulani lakini ukapata matokeo mabaya tofauti na matarajia yako.
“Binafsi naamini ligi yetu inazidi kuwa ngumu kadri miaka inavyozidi kwenda, msimu huu timu zimejipanga sana licha ya kuwepo kwa changamoto mbalimbali za kifedha na kiutawala, kama misimu inayokuja itakuwa hivi hakika kupata nafasi tatu za juu itakuwa shughuli pevu”. Alisema Mexeme.
Kocha huyo mwenye historia ya kuzikataa timu za Simba na Yanga wakati wake wa soka na kujikita na wakata miwa wa mashamba ya miwa ya Manungu Turiani aliongeza kuwa kikosi chake msimu huu kimechanganya damu changa na wakongwe.
“Vijana wangu wanacheza vizuri na kuleta matumaini ya kufanya makubwa siku za usoni, wakongwe pia wanaonesha kiwango kikubwa hivyo naweza kusema kuwa wachezaji wote wanacheza vizuri sana”. Alisisitiza Mexme.
Mexime mwenye sifa ya uzalendo aliongeza kuwa kwa sasa hesabu zake ni kushinda mchezo wa funga pazia la ligi kuu msimu wa 2012/2013 dhidi ya maafande wa Jeshi la Kujenga taifa kutoka mkoani Pwani JKT Ruvu mei 18 mwaka huu uwanja wa Chamazi uliopo Mbande nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.
“Nafikiri mechi ya mwisho ni muhimu sana, natarajia kuibuka na ushindi kutokana na maandalizi mazuri ninayofanya hapa Manungu, baada ya hapo nitakaa chini na kuandika ripoti yangu kwa ajili ya msimu ujao wa ligi”. Alisema Mexme.
Mchezo uliopita kocha huyo aliiongoza Mtibwa kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya vibonde wa ligi hiyo Africa Lyon ambao kwa sasa wanaweza kutoa mkono wa bai bai kucheza ligi hiyo na kuanda zao ligi daraja la kwanza.
Mabao yote katika mchezo huo yalifungwa na nyota wao anayekodolewa macho na baadhi ya timu vigogo ili kuinasa saini yake msimu ujao, Hessein Javu.
Uwezo wa kufumania nyavu wa Nyota huyo, nidhamu ya mzaoezi na umakini wa kucheza na nafasi ndio siri kubwa ya kupata mfanikiao klabuni hapo.
Mtibwa Sugar kwa sasa wapo nafasi ya sita wakiwa na pointi 39 sawa na Simba lakini wanazidiwa wastani wa mabao ya kufunga na kufungwa

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video