Monday, May 6, 2013

SIMBA

Na Baraka Mpenja
Mabingwa wapya wa ligi kuu Tanzania bara klabu ya Yanga ya Dar es salaam “Wazee wa Uturuki” wanaendelea kuimarisha mawindo yao juu ya watani zao wa jadi waliovuliwa taji msimu huu, wekundu wa Msimbazi Simba “Taifa kubwa” utakaopigwa uwanja wa taifa jijini Dar es salaam mei 18 mwaka huu.
Afisa habari wa klabu ya Yanga, Baraka Kizuguto ameimbia MATUKIO DUNIANI kuwa wachezaji wanaisubiri kwa hamu mechi hiyo ambayo ni maalumu kwao kunogesha ubingwa wao walioutwaa msimu huu kwani wasiposhinda mechi hiyo taji lao litaingia shubiri.
“Tunaendelea vizuri na mazoezi, wachezaji wote wapo salama na tunahitaji ushindi katika mchezo wetu wa mwisho ambao tutapambana na watani wa jadi Simba ambao mechi za mwisho wanakuja vizuri, lakini tunaimarisha mawindo yetu”.  Alisema Kizuguto.
Kizuto alisisitiza kuwa Yanga wamejipanga sana msimu huu na kuwazuia katika mchezo wowote ule ni kazi ngumu sana.
Afsia habari huyo alisema wachezaji wa Yanga “Watoto wa Jangwani na Twiga” wamekuwa wakiambiwa kuwa raha ya ubingwa ni kumpiga mtani wako, hivyo maandalizi ni mazuri na lazima washinde mechi hiyo ya mwisho.
“Kila mchezaji wetu anajua wajibu wake, Simba ni timu nzuri na vijana wao wanacheza kwa uzuri, lakini sisi tunajipanga barabara”. Alisema Kizuguto.
Pia alisema Yanga inayoongozwa na wachezaji nyota kama Haruna Hakizimana Fadhil Niyonzima, Khamis Kiiza, Frank Domayo, Simon Msuva na wengine wengi itacheza soka safi na la kuvutia mbele ya maelfu ya mashabiki wa klabu hizo.
Wakati Yanga wakijiwinda na mechi hiyo, Simba waliopo nafasi ya tatu wakijikusanyia pointi 42 kibondoni baada ya kushinda mchezo wa jana dhidi ya Ruvu Shooting mabao 3-1 uwanja wa taifa, wao wamebakiza mechi mbili ambapo kesho kutwa jumatano watashuka dimbani kuvaana na maafande wa Mgambo JKT kutoka jijini Tanga.
Kwa mujibu wa kocha msaidizi wa Simba Jamhuri Kiwhelu “Julio Alberto”, alisema kwa sasa timu inaandaliwa kwa ajili ya mchezo wa kesho kutwa na baada ya hapo watahamishia akili zao katika mchezo wa watani wa jadi mei 18 mwaka huu.
“Kila mtu anaona maendeleo ya timu, vijana wanaimarika kila mechi, nadhani mechi  dhidi ya Yanga tutawafunga na kubakisha heshima yetu pale pale”. Alisema Julio.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video