Friday, May 3, 2013

12

Na Baraka Mpenja
 Michuano ya vijana kwa umri wa miaka chini ya  12 (under 12)  na 14 (under 14)  inayosimamiwa na chama cha soka la vijana wilaya ya Ilala (IDYOSA) inatarajiwa kuanza kutimua vumbi hapo kesho (mei 4) katika dimba la kumbukumbu ya Karume Ilala jijini Dar es salaam.
Mwenyekiti wa IDYOSA Faza Edwirn Mloka ameiambia MATUKIO DUNIANI kuwa maandalizi yote yamekamilika na kinachosubiriwa ni muda kufika ili mashabiki wa kandanda washuhudie vipaji vipya kwa vijana ambao watalibeba taifa siku za usoni.
 “Michuano imeandaliwa kwa uzuri sana na matumaini yetu ni ushindani mkubwa kwa timu shiriki huku kanuni na sheria 17 za mchezo wa soka zikitumiwa”. Alisema Mloka.
 Mloka aliongeza kuwa tayari waamuzi wameshapangwa tayari kwa kuanza kwa mitanange hiyo ya mayoso.
 “Kwa sasa soka la vijana ndio msingi wa taifa lolote lile duniani, tumeshazalisha vijana wazuri kama Abubakar Salmu “Sure Boy” na Frank Domayo, hakika ni mavuno ya michuano hii, wadau wajitokeza kwa wingi kushuhudia vijana wadogo wakifanya vizuri”. Alisisitiza Mloka.
 Kwa upande wake katibu mkuu msaidizi wa IDYOSA Saidi Pamballelo alisema kwa mwaka huu timu zote zimejipanga vizuri kutokana na kupata muda mrefu wa maandalizi.
Pia Pamballelo ametaja ratiba ya kesho na kesho kutwa kama ifuatavyo;
 Tarehe 4/05/2013.
1.stone city (vs) new team
2.makoba (vs) home team
3.kulasini orphans center  (vs)  bom bom
4.vumbua vipaji ( vs) real boys
 Ratiba  ya tarehe 5/may/2013  siku ya jumapili
1.toto f.c (vs) e elimu .f.c
2.amana shooting( vs)  barcerona
3.kinota f.c  (vs) nuru .f.c
4.kinota  (vs) tabata rangers
 Aidha Pamballelo aliongeza kuwa wao wamejipanga vizuri na kuzingatia sheria zote na mwaka huu hakuna vijeba kwani timu zote zilifanyiwa usaili makini sana.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video