Monday, May 6, 2013

2
Na Anna Nkinda – Kuwait
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete amekiomba kituo cha watoto wenye mtindio wa Ubongo kilichopo nchini Kuwait kushirikina na Tanzania ili waweze kufanya kazi kwa pamoja ya kuwasaidia na kutoa mafunzo kwa watoto wenye matatizo kama hayo waliopo nchini. 
Mama Kikwete alilitoa ombi hilo jana alipotembelea kituo hicho kwa ajili ya kuona jinsi wanavyotoa mafunzo kwa watoto hao ambayo yameweza kuwabadilisha akili zao  na kuwa sawa na za watu wengine.
Alisema kuwa watoto wenye mtindio wa ubongo hata nchini wapo na wanapata mafunzo katika vituo vichache zilivyopo lakini kama watashirikiana kwa pamoja wataweza kubadilishana ujuzi ambao utawasaidia kutoa  mafunzo mazuri zaidi kwa watoto hao.
“Ninawapongeza kwa  kwa kazi kubwa na nzuri  mnayoifanya ya kutoa mafunzo kwa watoto hawa kwani  ni jambo jema  kuwasaidia watu wenye matatizo.
 “Watoto hawa wakipewa mafunzo akili yao itakuwa sawa na watu wengine, wakiwa wakubwa na kufikia umri wa kujitegemea wataweza kufanya kazi mbalimbali za maendeleo ambazo zitawaingizia kipato na  kuwasaidia katika maisha yao ya baadaye”, alisema Mama Kikwete.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kituo hicho Dk. Samira  Al-Saad alisema kuwa kama watoto wenye matatizo ya mtindio wa ubongo watapelekwa   shule mapema zinazotoa mafunzo kwa ajili yao  watapona na kuwa na  akili sawa na watu wengine.
Dk. Samira alisema kuwa wazazi wengi hawajui kwamba matatizo ya mtindio wa ubongo yanatibika kama mtoto akipewa elimu ya darasani na kufanyishwa mazoezi ambayo yatamsaidia kufanya  shughuli zake mwenyewe bila ya kutegemea msaada wa jamaa zao.
“Kituo hiki  kilifunguliwa mwaka 1994 na hadi sasa kina wanafunzi  120  ambao wanapata mafunzo ya nadharia na vitendo na kinajiendesha kwa kupata msaada kutoa Serikalini, watu na mashirika binafsi ya ndani na nje ya nchi”, alisema Dk. Samira.
Aliendelea kusema kuwa umri wa watoto wa kuanza masomo ni  miaka sita  hadi 15 na kama mwanafunzi atakuwa amevuka miaka 15 atajifunza zaidi mafunzo ya vitendo ambayo yatamuwezesha kujitegemea hapo baadaye.
Dk. Samira alisema, “Wanafunzi wetu wameweza kupata ajira sehemu mbalimbali hii ni baada ya kupata mafunzo ambayo yamewafanya kuwa na akili sawa na watu wengine ambao hawana matatizo haya, kuna baadhi yao tumewaajiri hapa na hivi  sasa wanawafundisha wanafunzi wenzao.
Mama Kikwete pia alitembelea Kituo cha Al-Kharafi ambacho kinatoa huduma ya mazoezi kwa watoto wenye matatizo ya mtindio wa ubungo  na kuona jinsi watoto hao wanavyofanya mazoezi yao.
Kituo hicho kinapokea  watoto wenye umri wa kuanzia miaka minne hadi  12 ambao wanafanya mazoezi kwa kucheza michezo mbalimbali ambayo inawabadilisha akili zao na kuwa katika hali ya kawaida .
Akiwa katika kituo hicho alijionea kazi mbalimbali zinazofanywa na watoto hao ambazo ni  uchoraji, ushonaji, upishi  pia aliona michezo mbalimbali ikiwa ni pamoja na nyimbo na maonyesho ya mavazi.
Mama Kikwete aliambatana na  Mumewe  Rais Jakaya Mrisho Kikwete nchini Kuwait kwa ziara ya kikazi ya siku mbili.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video