Wednesday, May 1, 2013

Madiwani wakimsikiliza mwenyeki wa Halmashauri MKITI 11Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji mpanda akitoa maamuzi ya kikao cha madiwani kwenye ukumbi wa chuo kikuu huria cha kumwazimia Mkurugenzi wao Picha zote na ((Kibada Kibada Katavi.)

Na Kibada Kibada –Mpanda Katavi.
Sakata la halmashauri ya mji wa mpanda lililokuwa likiigubika Halmashauri hiyo kwa muda mrefu la  kumkataa Mkurugenzi wa Mji wa Mpanda Joseph Mchina limeingia katika hatua nyingine kufuatia madiwani wa Halmashauri hiyo kuitisha kikao cha baraza  maalumu  la  madiwani la kuiomba    Serilali  kumuhamisha  mkurugenzi huyo kutokana na tuhuma mbalimbali zinazomkabili.
Akizungumza katika kikao hicho Mwenyekit Halmashauri ya mji wa Mpanda  Enock Gwambasa alisema baraza hili liligeuka na kuwa kamati maalum kwa ajili ya kujadili tuhuma mbalimbali zinazowakabili watumishi kwa kufuata taratibu kanuni na sheria za kiutumishi na kufikia maamuzi ambapo waliomba serikali kumhamisha mkurugenzi wa mji  haraka iwezekanavyo  kufuatia  baraza hilo  la madiwani kumkataa  kutokana na   na tuhuma mbalimbali  zinazomkabiri zikiwemo   za  matumizi mabaya ya fedha na mali  za Halmashauri iliyosababishia kuipatia hati yenye mashaka kwa kipindi cha miaka miwili mfululizo.
Tamko  hilo la baraza  la madiwani  lilitolewa  jana  kwenye  kikao chao  kilicho  fanyika  kwenye ukumbi wa mikutano wa Chuo Kikuu Huria  Tawi la  Mkoa wa Katavi  na kuhudhuriwa na watalaam pamoja na wageni  waalikwa.
Baraza hilo   Maalumu la Madiwani  lilifanyika  kufuatia  maamuzi yaliyo  pitishwa na Baraza la Madiwani  yaliyotolewa kwenye kikao   cha  Aprili  4 mwaka huu  ambacho  kilipanga kuitishwa kwa kikao maalum ndani ya siku 21  ili kumjadili Mkurugenzi   kutokana  na tuhuma  saba zilizo kuwa zikimbabili
Katika Kikao hicho  kilianza  kwa Mwenyekiti  wa Halmashauri  YA Mji wa Mpanda Enock Gwambasa  kuwaeleza wajumbe  wa baraza kuwa  kikao   kilikuwa kifanyika siku moja kabla  yaani April 29, lakini  Katibu  Tawala wa Mkoa   Mhandisi Emanuel Kalobelo  aliwaandikia barua ya kusitishwa kwa kikao hicho  kwa kile kilichoelezwa  kukiukwa kwa  kwa utaratibu  wa  kikao   namna ya kuitisha Maraza Maalumu la Madiwani  la kumjadili Mkurugenzi wao.
Mwenyekiti Gwambasa aliendelea kueleza kuwa  hata hivyo baada ya mjadala mrefu  baina  ya Katibu Tawala na  Madiwani  walikubaliana  kikao   kifanyike siku iliyofuata yaan April 30 kwa kufuata  kakuni,taratibu sheria na   miongozo  zinavyoelekeza.
Kikao    cha kamati ya Madiwani kilichukua mwendo wa saa 3  kusikiliza na kujadili tuhuma   na kisha  madiwani   walikaa tena  kama Baraza  na kutowa  tamko lao  lilitolewa na Mwenyeki wa Halmashauri Enock Gwambasa kwa niaba ya madiwani
Mwenyekiti  alieleza kuwa Baraza  limefikia uamuzi wa kuiomba  Serikali  imuhamishe kwa kumpangia kituo   kingine cha kazi  Mkurugenzi  Joseph Mchina kwa kuwa  wao madiwani  hawamtaji  katika Halmashauri yao.
Akifafanua zaidi Gwambasa lisema maamuzi ya kikao hicho  watapelekwa  ngazi husika   za juu  ili  ziweze  kufuatilia tatizo la  Mkurugenzi  huyo na kuchukua hatua kwa kufuata taratibu za kiutumishi.
Alizitaja miongoni mwa  tuhuma anazotuhumiwa nazo Mkurugenzi    Mchina   kuwa  ni matumizi mabaya ya fedha za Halmashauri hali iliyosababisha Halmashauri kupata hati yenye mashaka miaka miwili mfululizo,pia wamekuwa wakitoa maelekezo lakini hayatekelezwi.
Kwa upande wake  Joseph  Mchina  alipoulizwa ameupokeaje uamuzi huo habari wa baraza  la madiwani alisema  kwa kuwa mambo haya yanakwenda kwenye ngazi za juu za Serikali ni vyema kusubiri    Serikali itatowa maamuzi gani kwani mapema mno kuzungumzia.
Mbunge wa jimbo  la Mpanda Mjini Said Arfi akizungumzia  uamuzi wa uliochukua na baraza la madiwani nayeye akiwa sehemu ya madiwani kwa mjibu wa sheria kwa kuwa ni Mbunge wa jimbo la mpanda Mjini alieleza kuwa ni sahihi  na wao wameongozwa na kanuni zao .
Wao wamependekeza Mkurugenzi ahamishwe kwa kuwa amekaa kwenye kituo hicho kwa muda mrefu hivyo amekuwa akifanya kazi kwa mazoezi amekaa mpanda tangu mwaka 2003 alipokuwa Afisa Utumishi kuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji hadi Mkurugenzi hivyo ni vyema akabailisha kituo cha kazi hapo hata utendaji katika halimashauri utabadilika kwa kuwa kuna mazoea ya muda mrefu.
Pia akashauri zana ya kutelemsha madaraka kwa wananchi kuwa ni muhimu kwa bado sehemu hiyo hajapatiwa umuhimu madiwani wakawa na maamuzi yao yakiwa na nguvu kuliko hadi kusubiri maamuzi kutoka juu.hivyo moja ya mapendekezo waliyoyatoa katika kikao ni vyema wakamhamisha kutoka kituo kimoja hadi kingine ili kubadilisha utendaji kazi.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video