Wednesday, May 22, 2013

Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
Kiungo  mkongwe na kipenzi cha mashabiki wa timu ya taifa ya Engaland na klabu ya Chelsea ya jijini London, Muingereza Frank James Lampard amesema kamwe hajawahi kuwa na mahusiano ya karibu sana na kocha wa muda wa klabu hiyo anayemaliza mkataba  wake mwishoni mwa mwezi huu, Rafa Benitez.
Rafa aliyechukua mikoba ya aliyekuwa kocha kipenzi kwa mashabiki wa Chelsea, Roberto Di Matteo ambaye alifukuzwa mwaka jana na mmiliki wa klabu hiyo Roman Abramovich anasemekana kutokuwa na tabia ya kuwa na mahusiano ya karibu sana na wachezaji wake.
Leo hii kiungo Lampard ameeleza kuwa kocha huyo ambaye amekuwa akipingwa na mashabiki wa klabu hiyo katika muda wake aliokaa klabuni hapo, kamwe hajawahi kuwa na mahusiano na yeye pamoja na wachezaji wote wa Chelsea.
“Siku zote Benitez amekuwa mtu wa mapambano na kujituma sana, ana uvumilivu mkubwa sana, binafsi sijawahi kuwa chanzo cha yeye kuwaza vibaya, lakini kitendo cha mashabiki wetu kumpinga  ni udhaifu wa kibinadamu, anatakiwa kuwasamehe”. Alisema Lampard.
Lampard aliongeza kuwa kuna makocha ambao unaweza kuwa na mahusiano ya karibu na kujihisi kama mtu wako wa karibu kwako, lakini Rafa huyuko hivyo kwani anapenda zaidi kufanya mambo yake.
“Kiukweli sio kocha wa kukaa naye chini mkaongea”. Alisema Lampard.
Nyota huyo alimsifu Benitez kwa kuwa na uwezo mkubwa wa kuandaa timu kwa ajili ya mechi na kumfananisha na kocha Fabio Capello aliyekuwa kocha wa timu ya taifa ya Uingereza “Simba watatu”.
Benitez amewapa Chelsea ubingwa wa ligi ya Uropa na kufuzu kucheza ligi ya mabingwa msimu ujao, lakini mkataba wake unaisha mwishoni mwa mwezi huu.
Distance: Frank Lampard says he has never formed a tight relationship with Rafa Benitez 
Frank Lampard amesema hajawahi kuwa na mahusiano ya karibu na kocha wake Rafa Benitez
Lampard  amepewa mkataba mwingine wa mwaka mmoja darajani baada ya kuwepo kwa wasiwasi mkubwa kuwa  angemalizana na klabu hiyo

Nyota huyo mpaka sasa anashikilia rekodi ya kuifungia Chelsea mabao mengi zaidi ambapo mpaka sasa ametia kambani mabao 203 huku akitarajiwa kuichezea klabu yake chini ya kocha Jose Mourinho msimu ujao.
On target: Benitez achieved his objectives of qualifying for the Champions League and winning a cup
 Benitez amefanikiwa kufuzu kucheza ligi ya mabingwa na kutwaa kombe la Uropa mwaka huu
New deal: Lampard has secured himself another year with Chelsea 
MKATABA MPYA: Lampard  ameongezewa mkataba mpya wa mwaka mmoja kuichezea Chelsea

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video