Saturday, May 4, 2013

MASHABIKI JUU
Na Baraka Mpenja
Michuano ya Singaone Cup imeanza kushika kasi manispaa ya Songea mkoani Ruvuma kwa mchezo wa ufunguzi wa kundi A kupigwa leo hii.
Katika mchezo huo klabu ya Bombili ilishuka ugani kumenyana na Soccer City na kushuhudia  City wakibuka kidedea baada ya kuwalaza wapinzani wao bao 1-0.
Kipute hicho kimetajwa kuchezwa kwa ufundi mkubwa huku kila timu ikisaka pointi tatu dakika hizi za mapema kwani ujanja ni kuwahi mapema.
Mdhamini mkuu wa mashindano hayo Bwana Golden Singaone ambaye ni mwenyekiti wa chama cha soka mkoani Ruvuma (FARU) ameimabia MATUKIO DUNIANI  kuwa ufunguzi wa mashindano hayo ambayo hufanyika kila mwaka ulikuwa wa aina yake kutokana na watu wengi kujitokeza leo hii.
“Hakika nimeridhishwa sana na mahudhuria ya wadau wa soka na mashabiki wote, wamefika kwa wingi sana na kufanya mashindano ya mwaka huu yaanze kwa kishindo”. Alisema Singaone.
Singaone aliongeza kuwa mashindano hayo yanajumuisha timu za manisapaa ya Songea tu, lakini anafikiria kuyapanua zaidi ili kuyafikia maeneo mengi zaidi.
“Ukiangalia mikoa mingi soka linachezwa mjini, mimi nafikiri mkoani kwangu imefika wakati wa kufuta suala hilo, nadhani nitajipanga kushirikiana na wadau wengine kuyafikia maeneo yote ya Ruvuma”. Alisisitiza Singaone.
Mwenyekiti huyo alisema licha ya yeye kuwa mwanasiasa ameamua kujiingiza katika mchezo wa soka kwani unawavutiwa watu wengi zaidi duniani kote.
Baada ya kipute cha ufunguzi leo hii baina ya Bombili na Soccer City, Singaone alisema hapo kesho michuano hiyo itaendelea kwa timu za Kundi B kushuka dimbani ambapo Nastboys watakwaana na Magereza majira ya saa kumi kamili jioni.
Aidha Singaone aliwataka mashabiki wa soka kuendelea kujitokeza kwa wingi ili kushangilia timu zao na kupata burudani ya soka.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video