Saturday, May 4, 2013

1
Kipre Herman Tchetche akimtoka kwa ufundi mkubwa beki wa FAR Rabat mchezo wa kwanza Dar es salaam

Na Baraka Mpenja
Mabingwa mara mbili mfululizo wa kombe la mapinduzi, makamu bingwa wa kombe la kagame na ligi kuu msimu uliopita, klabu ya Azam FC  “wana lambalamba” ya jijini Dar es salaam chini ya kocha Mwiingereza Sterwat John Hall,  leo hii majira ya saa 11 jioni kwa saa za Morroco ambapo itakuwa saa moja usiku kwa saa za afrika mashariki wanatarajia kushuka dimbani dhidi ya AS FAR Rabat ya huko katika mchezo wa marudiano wa raundi ya tatu kombe la shirikisho.
Mchezo huo unatarajia kuwa wa kukata na shoka kutokana na uwezo mkubwa walionao Azam pamoja na FAR Rabat, lakini matokeo ya mchezo wa kwanza jijini Dar es salaam wiki mbili zilizopita uliomalizika kwa suluhu pacha ya bila kufungana yanaweza kusababisha mechi ikawa ngumu zaidi.
Waarabu tabia yao inayojulikana sana ni kutafuta matokeo ya sare ama suluhu ugenini na kumalizia kibarua wakiwa kwao.
Wakiwa Dar es salaam walifanikiwa kutumia mbinu hiyo na kulazimisha suluhu mbele ya Azam, na leo hii wanatafuta njia ya kuwachinjia mbali wana lambalamba wanaoshika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi kuu Tanzania bara wakijikusanyia pointi 48.
Katika mchezo wa leo matokeo ya sare ya mabao yoyote ama ushindi utawapa nafasi Azam kusonga hatua ya makundi ya kombe la shirikisho.
Kama timu hizo zitaenda suluhu tena itatumika sheria nyingine kupata mshindi wa kusonga mbele ambayo nikupigiana mikwaju ya penati ama matuta.
Azam kwa kutambua fitina za waarabu ambao wanatabia ya kufanya umafia wakiwa nyumbani kwao walienda huko mapema na kuweka kambi ya wiki moja ili kuangalia mazingira ya huko na kuzoea mambo yao mapema.
Kuwahi kwenda Morroco kumewapa nafasi ya kujua mengi na kujiandaa na mchezo huo huku wakikabiliana na presha kubwa ya mashabiki wa Morroco wenye hasira na Tanzania baada ya timu yao ya taifa kufungwa na Taifa stars mabao 3-1 katika mchezo wa kuwania kufuzu fainali ya kombe la dunia.
Leo hii azam ikiwa na kikosi cha wachezaji mahiri kama Kipre Herman Tchetche, John Rafael Bocco, Hamis Mcha “Vialli”, Abubakar Salum “Sure Boy”, Jabir Aziz “Stima”, Brian Umony, Hamphrey Mieno, Himid Mao, Michael Bolou , David Mwantika, na wengine wengi wana matumaini makubwa ya kuwafunga wenyeji wao na kuwapa raha watanzania ambao kwa sasa wamezoeza raha za Taifa stars.
Pia ufundi mkubwa wa kocha Hall unaweza kuwabeba matajiri hao wa Tanzania na kusonga hatua inayofuata.
Kila la Heri Azam Fc, Mungu Ibariki Tanzania Mungu Ibariki Azam fc.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video