|
|
Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Supersport.com
Rais
wa chama cha soka nchini Zambia FAZ Kalusha Bwalya amefurahiswa na
kurejea kwa michuano ya ukanda wa nchimwanachama wa baraza la michezo
kusini mwa Afrika COSAFA ambayo itafanyika mwaka huu nchini Zambia.
Kalusha alisema michuano hiyo
mikubwa itawasaidia wachezaji wa ukanda huo kushindana kwa nguvu, na
Zambia kupewa heshima ya kuwa mwenyeji wa michuano hiyo hakika ni
heshima kubwa sana kwao.
“Nimefurahishwa na urejeo wa
michuano hii, zambia kuwa mwenyeji ni furaha kubwa sana, tumesubiri sana
nafasi hii na kuwa mwenyeji imetupa heshima zaidi”. Kalusha ameuambia
mtandao wa Superspot.com
Pia
aliongeza kuwa michuano hiyo itatoa nafasi kwa wachezaji kushindana
kiundugu sanjari na kujulikana kutokana na michuano hii kurushwa na
vituo mbalimbali vya runinga.
Kalusha alikuwa miongoni mwa wasemaji wakuu wa COSAFA katika draw iliyofanyika jijini Lusaka nchini Zambia.
Katika
michuano hiyo timu ya taifa ya Tanzania “Taifa stars” imealikwa
kushiriki na COSAFA na tayari shirikisho la soka nchini Tanzania TFF
limekubali mwaliko huo muhimu ambao utawakutanisha wachezaji wa Tanzania
na wachezaji wengine wa Kusini mwa Afrika.
Stars
itaenda kucheza michuano hiyo ikiwa tayari ilishakutana na Zambia
waliokuwa mabingwa wa soka barani Afrika kabla ya kuupoteza mwaka huu
nchini Afrika kusini na kuibuka na ushindi wa bao 1-0 liliLofungwa na
Mrisho Ngasa uwanja wa taifa mwezi Disemba mwaka jana.
0 comments:
Post a Comment