Thursday, May 16, 2013

1
Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe Dar es salaam

Licha ya kutokushuka daraja wala kuwania ubingwa ambao tayari upo mikononi mwa Yanga msimu huu, maafande wa JKT Oljoro wa jijini Arusha wametamba kuonesha kabumbu maridhawa kesho kutwa katika uwanja wa Shekh. Amri Kaluta Abeid dhidi ya Azam Fc kutoka Dar es salaam.
Kocha msaidizi wa maafande hao Riziki Shawa ameimabia MATUKIO DUNIANI kuwa maandalizi yanakwenda vizuri na lengo lao ni kutoa burudani kubwa kwa mashabiki wao ambao wamewaungana mkono sana msimu huu.
“Awali ya yote tunamshukuru Mungu aliyetupa uzima mpaka siku ya leo, sisi tumejiandaa vizuri kuwavaa Azam, mchezo utakuwa mzuri sana”. Alisema Shawa.
Kocha huyo alisema mchezo huo hauna mchecheto mkubwa sana kwani wao hawashuki daraja wala hawahitaji ubingwa, kikubwa wanahitaji burudani na kupata ushindi wa kuhistoria.
“Azam ni timu nzuri, imetoka kucheza mashindano ya kimataifa na wanajiamini zaidi, sisi Oljoro hatuna wasiwasi kutokana na maandalizi yetu”.
Shawa aliwataka mashabiki wa Arusha kujitokeza kwa wingi katika mchezo huo kwani wamejiandaa kuonesha kandanda la kufa mtu na kila atayekuwepo siku ya mechi uwanjani hatajuta kutoa kiingilia kutazama mechi hiyo.
Kocha huyo mwenye historia ya kulijua soka la Tanzania aliongeza kuwa wakishinda watafikisha pointi 32 na hii itatoa nafasi nzuri ya kujipanga zaidi msimu ujao ili kupata nafasi tatu za juu.
Pia Shawa alisisitiza kuwa katika mchezo huo watawatumia baadhi ya vijana wao ambao wanaamini wataleta ushindani mkubwa.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video