Saturday, May 18, 2013


Mpepetano wa watani wa jadi, Simba vs Yanga  mechi za nyuma  watani 
Okwi (kushoto) alikuepo mechi ya msimu wa mwaka jana na safari hii hayupo, Simba bila yeye itaweza?

Na Baraka Mpenja
Kwa wale wenye roho nyepesi watapata shida kubwa sana katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam kuanzia majira ya saa 10 kamili jioni ambapo mwamuzi Martin Saanya kutoka Morogoro atapuliza kipenga kuashiria kuanza kwa pambano la kukata na shoka, kukata na mundu baina ya watani wa jadi, wekundu wa Msimbazi Simba “Taifa Kubwa” dhidi ya mabingwa wapya wa ligi kuu soka Tanzania bara, Dar Young Africans.
Langoni kwa Simba asilimia kubwa Juma Kaseja anaweza kuanza au Abeid Dhaira, yeyote atakayeanza lango la Simba litakuwa salama.
Kwa Yanga Ally Mustapha “Bartez” kwa mara ya kwanza ataidakia Yanga katika mechi ya watani wa jadi, ni kipa mwenye uwezo mkubwa na leo hii atasimama langoni huku mpinzani wake mkubwa Kaseja naye akiwa kibaruani.
Kwa upande wa Simba, walinzi Masoud Nasoro Chollo anaweza kuanza kulia, kushoto Miraj Juma na katikati Musa Mudde na Shomary Kapombe. Katika safu hii ya ulinzi mchezaji ambaye hajawahi kukumbana na presha ya pambano la watani wa jadi ni Miraj Juma pekee, wengine wote wanauzoefu mkubwa na wanaweza kusimama kidete, lakini huyu kinda anatulia sana na huwa hababaishwi  na mafaza.
Ukuta huu ambao ni bora utakuwa unakabiliana na wachezaji wa Yanga kati ya Said Bahanuz, Jerry Tegete, Didier Kavumbagu na Hamis Kiiza, ambao yeyote anaweza kuanza katika mchezo  wa leo. Itakuwa burudani kubwa sana.
Kwa beki ya Yanga Mbuyu Twite anaweza kuanza kulia, kushoto Oscra Samwel Joshua au David Luhende, na ngome ya kati, injinia Kelvin Patrick Philip Yondan na Nadir Haroub “Canavaro” watasimama.
Ukuta huu utakumbana na presha kubwa kutoka kwa nyota wa simba ambao watapangwa na kocha wao, inawezekana akaanza Amri Kiemba ambaye hatabiriki atacheza wapi au Ramadhan Singano “Messi” .
 Viungo watachuano kufa mtu, kwa upande wa Mnyama, Musa Mude anayecheza chini na mbele yake husimama Abdallah Seseme “Dullah” au Mwinyi kazimoto Mwitula huku viungo wa pembeni wakisimama wachezaji wawili wenye kasi kubwa sana Mrisho Khalfan Ngasa “Anko” na Haruna Chanongo.
Kwa Upande wa Yanga,Athman Idd “Chuji” atacheza chini, juu yake Domayo, kulia Simon Msuva na kushoto Haruna Hakizima Niyonzima.
Wachezaji wote hao wamekamilika sana na wana uwezo mkubwa wa kucheza soka, na leo hii itakuwa raha kubwa sana uwanja wa taifa.
Watu wengi wanaipa Yanga nafasi ya kushinda kwa madai kuwa inawatumia wachezaji wote wenye uzoezfu na mechi ya watani wa jadi, wakati Simba inawatumia vijana wao waliowapandisha kutoka timu B.
Hakuna ukweli, Mnyama kikosi chake kimechanganya damu na kina wachezaji vijana walioaminiwa na kocha Mfaransa Patrick Liewig kutokana na uwezo wao wa kucheza soka.
Timu yoyote inaweza kuibuka na ushindi, endapo Yanga watawadharau Simba kwa kutumia vijana wao, watakwenda na maji na pengine kutibuliwa sherehe zao za kukabidhiwa kombe.
Kwa upande wa Simba walishapoteza ubingwa na wanahitaji heshima mbele ya watani wao wa jadi, hivyo wamejiandaa kwa uzuri sana kupambana na Yanga yenye wachezaji wazuri sehemu zote na wamekaa pamoja kwa muda mrefu, walienda hadi Uturuki, si mchezo kwa kweli.
Nao Simba walienda Oman ingawa ziara yao haijawanufaisha sana, lakini bado si haba, kikosi wanacho na wanaweza kupata ushindi leo kama wataamka vizuri.
Kila upande umejigamba sana kwa takribani wiki moja ya maandalizi, hatimaye saa zazidi kuyoyoma na leo hii saa 10 kamili kipute kinaanza uwanja wa taifa.
Mwenye macho haambiwi Tazama, kama uko njema mfukoni, jiandae kwenda uwanja wa taifa, na mechi hiyo itatumiwa kugawa zawadi kwa washindi, hivyo kutakuwepo na hafla fupi ya zoezi hilo.
Bingwa ni Yanga, nafasi ya pili ni Azam fc ambao leo hii watakuwa Arusha, na nafasi ya tatu wapo Simba, kama ilivyokuwa kwa Yanga msimu uliopita.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video