Askofu msaidizi Kanisa katoliki wa Jimbo kuu la Dar Es Salaam Mhashama Euseblus Nzigirwa akizungumza katika Harambee hiyo
Bw.Justine Nyenza ambae alizaliwa tarehe kama kituo
cha Radio Maria akikata keki kama ishara ya kusherekea tangu kuanzishwa
kwa Radio hiyo. wakati wa sherehe za miaka 17 ya Radio Maria na
harambee ya kuchangia mipangilio ya vipindi ilifanyika jana katika
ukumbi wa Msimbazi Center jijini Dar es salaam.
Na Philemon Solomon
Wito umetolewa
kwa Watanzania wote nchini kusikiliza au kusoma habari za kujenga na
zenye maadili kwa Jamii inayowazunguka ili kujenga maadili ya kimwili na
kiroho.
Akizungumza
Askofu msaidizi Kanisa katoliki wa Jimbo kuu la Dar Es Salaam Mhashama
Euseblus Nzigirwa amesema watanzania wengi wanapenda kusikiliza habari
mbaya za kubomoa kuliko kusikiliza habari za kufundisha, hivyo amewataka
wazazi na walezi waanze pamoja na watoto kusikiliza vipindi vinavyo
fundisha kimwili kiroho na kiadilifu.
Mhashamu
EUSEBIUS ameongezea kwa kusema kuwa kutokana na hali ya sasa ya bungeni
ilivyo jitokeza kwa kurushiana maneno yasiyo faa na wakati wao ni watu
wazima imeonekana kama wakati wabunge hao wakiwa watoto hawakupata
malezi yasiyofaa, hivyo imepelekea watu kuona hizo kauli chafu za
wabunge wamejifunzia toka nyumbani wakiwa watoto ndiyo maana leo
wanazitoa bila kujali.
0 comments:
Post a Comment