Monday, May 20, 2013

Mrisho Khalfan Ngassa “Anko” atambulishwa jangwani, asaini mkataba wa miaka miwili NGASSA YANGA 
Siku ya mechi ya watani wa jadi mashabiki wa Yanga walimbeba Ngassa na kumvulaisha jezi ya Yanga

Na Baraka Mpenja
Siku mbili baada ya kumalizika kwa msimu wa Ligi Kuu soka  ya Vodacom Tanzania Bara, pilikapilika za usajili zimeanza na mabingwa wa ligi hiyo, Wanajangwani Dar Young Africans wameanza kwa kasi kubwa  baada ya kumsainisha mkataba wa miaka miwili nyota wa Simba mwenye kasi zaidi Mrisho Khalfan Ngassa “Anko”.
Ngasa alikuwa anacheza kwa mkopo katika klabu ya Simba SC akitokea kwa wana Lamba Lamba Azam FC na leo hii ametambulishwa rasmi mitaa ya Jangwani na Twiga kuichezea klabu yake hiyo ya zamani tangu aondoke miaka mitatu iliyopita.
Wakati Ngassa akiwa anarejea Jangwani, habari zaidi zinasema kwamba Simba SC nayo imepanga kujibu mapigo kwa kumsajili kiungo wa Yanga, Haruna Hakizimana Fadhil Niyonzima kwa dau la Sh. Milioni 70 walizokubaliana kwa mkataba wa miaka miwili.
Katibu mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako ameimbia MATUKIO DUNIAN kuwa klabu yao imeamua kumnasa Ngassa ili kuimarisha safu ya ulinzi ambayo imekosa mchezaji mshambuliaji wa kasi.
Mwalusako amesema nyota huyo bado yuko katika kiwango kizuri na atawasaidia sana wakati huu wa kampeni za kucheza ligi ya mabingwa barani Afrika mwakani.
“Safu ya ushambuliaji ni Simon Msuva pekee mwenye kasi zaidi, kwa sasa wakiungana na Ngassa hakika tutafanya vizuri sana”. Alisema Mwalusako.
Kuhusiana na taarifa za kumsajili Kapombe, Mwalusako amesema hawajazungumza kitu kwa sasa, lakini kama inawezekana wanaweza kumsajili.
Pia aliongeza kuwa sasa furaha ya mashabiki itakuwa kubwa kwani waliwaonesha dalili za kumhitaji Ngassa tangu siku ya mechi ya watani wa jadi mara baada ya kumvalisha jezi ya Yanga na kuonesha mabango ya kumtaka arudi jangwani.
“Tumefanikisha nia yetu, tumefurahi sana, naamini sasa Yanga inazidi kuwa tishio”. Alisema Mwalusako.
Mtandao huu umemtafuta mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba, Keptein Zacharia Hans Poppe ili kupata ufafanuzi kuhusiana na taarifa hiyo.
Poppe alisema wao hawana taarifa hiyo na wanashangaa kwa mchezaji huyo kusaini mkataba na Yanga wakati tayari ameshasaini mkataba wa mwaka mmoja kuichezea Simba msimu ujao.
“Mimi sijuia bwana, mkataba tulipeleka TFF na kama Yanga wamemsainisha leo  lazima wataupeleka TFF, sasa wenye maamuzi watabaki kuwa shirikisho”. Alisema Poppe.
Poppe aliongeza kuwa Yanga wamekuwa maarufu wa kutokufuata taratibu za usajili kwasababu hawajawaona Simba na kuongea chochote.
“Wangekuwa na busara wangekuja kuongea na sisi, lakini wanajifanyia tu mambo, kiukweli Ngassa bado ni mchezaji wetu”. Alisema Poppe.


 

Ngassa aliichezea Simba SC mechi ya 27 na ya mwisho Jumamosi katika kipindi cha kuwa kazini Msimbazi, wakati ilala mabao 2-0 mbele ya Yanga. Katika mechi 27 alizoichezea Simba SC, zikiwemo za Ligi ya Mabingwa mbili, kirafiki kadhaa na Ligi Kuu, Ngassa amefunga jumla ya mabao saba na kutoa pasi za mabao 13.

Baada ya mechi dhidi ya Yanga Jumamosi, mashabiki wa timu ya Jangwani walimfuata Ngassa na kumvalisha jezi ya timu hiyo, jambo ambalo lilichafua hali ya hewa kwa mashabiki wa Simba.
Ngassa alisajiliwa Azam Mei 21, mwaka 2010, kwa dola za Kimarekani 40,000, zaidi ya Sh. Milioni 60 kutoka Yanga SC, huku yeye mwenyewe akipewa dola 30,000, zaidi ya Sh. Milioni 45. 
Alitua Yanga kwa mara ya kwanza mwaka 2006, akitokea Kagera Sugar ya Bukoba, ambayo ilimtoa Toto African ya Mwanza.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video