Sunday, May 19, 2013

Mahojiano na Domayo yamefanywa na mmiliki wa blog hii, Baraka Mpenja na mwandishi wa mtandao wa Fullshangwe

Beki wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ (kushoto) akiwa na Frank Domayo na Simon Msuva wakati waki katika kambi ya Yanga nchini Uturuki.
Mipango ua kunyakua ubingwa ilianza baada ya kumalizika ka mzunguko wa kwanza ambapo Yanga walienda kuweka kambi ya wiki mbili nchini Uturuki na kurejea nchini kwa ahadi ya kutokupoteza mchezo hata mmoja. Domayo amesema hapo ndipo walipoanza kujiweka sawa na mafanikio kuonekana jana uwanja wa taifaY 
Sherehe za kushangilia taji la ligi kuu katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam huku wakiwa wamewaadhibi Simba mabao 2-0

Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe Dar es salaam
FULLSHANGWE: Hello! Frank Domayo!, Pole na uchovu wa mechi ya jana.
DOMAYO: Daah! Tumeshapoa anko, niambie Baraka?  mimi nipo kaka, unafikiri  Kuna cha kufanya basi! tunafurahia ubingwa wetu tu, napumzika tu hapa nilipo baada ya shughuli nzito ya jana.
FULLSHANGWE: Vipi Domayo baada ya kupangwa katika kikosi cha kwanza hapo jana na kuanza mechi ulikuwa unawaza nini?
DOMAYO: Eeeh! wee acha tu! nilikuwa nawaza jinsi ya kuisaidia timu yangu kushinda mchezo wa watani wa jadi, kama ulibyoona umati mkubwa kama ule. Haikuwa kazi rahisi kwangu.
FULLSHANGWE: Uliogopa mashabiki?
DOMAYO:Hapana, mimi nilichukulia Changamoto tu, nilikuwa sawa kwa lolote tu.
FULLSHANGWE: Baada ya kushinda mchezo wa jana dhidi ya Simba na kukabidhiwa Kombe umejisikiaje Domayo?
DOMAYO:  kiukweli! Binafsi nimefurahi sana kutwaa ubingwa wa kwanza wa ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2012/2013 nikiwa na klabu kubwa ya Dar Young Africans.
FULLSHANGWE: Jana ulikuwepo katika kikosi cha kwanza cha Yanga, ulijisikiaje?
DOMAYO:  Nilijisikaia furaha ikizingatiwa mechi ya jana ilikuwa ya mwisho na inatukutanisha na watani wetu wa jadi. Nilikuwa na furaha kutajwa kikosi cha kwanza ambacho kilikuwa na malengo ya kuongeza furaha zaidi ya kutwaa ubingwa msimu huu, nilijua raha itakuwa kubwa zaidi tukiwafunga Simba na imetokea hivyo.
FULLSHANGWE: Je, uliwahi kuwaza kuwa ipo siku utatwaa ubingwa na umri mdogo kiasi hicho?
DOMAYO: Yaah! Siku zote ilikuwa ndoto Yangu kuwa ipo siku nitatwaa ubingwa katika umri wangu mdogo na imetokea hivyo, daah! nimefurahi sana,  hata ndugu, jamaa na marafiki zangu wamefurahi sana na kunipongeza.
FULLSHANGWE: Ubingwa wa msimu huu unajenga picha gani kwako?
DOMAYO: Kaka unanipa somo kubwa sana, Unajua lazima ujue kitu kimoja kuwa kila mchezaji anapenda kutwaa vikombe, ubingwa wa msimu huu unanijengea picha ya kujipanga zaidi na kuitumikia klabu yangu kwa nidhamu kubwa ili kama namaliza umri wangu wa soka ije kubaki historia kwangu na kwa wanangu, au vipi bwana!!
FULLSHANGWE: Unamzungumziaje kocha Ernie Barandts aliyekupa nafasi muda wote?
DOMAYO:  Ni Kocha mzuri sana, anapenda sana wachezaji wazingatie nidhamu ya mazoezi na maelekezo yake, mara zote nimekuwa nikifanya kama kocha anavyotaka na ndio maana nimekuwepo katika kikosi cha kwanza kwa muda wote, najisikia furaha sana, kizuri chajiuza bwana! Nitakaza hivi hivi!
FULLSHANGWE: Msimu umeisha, utabaki kuwa Yanga au utaihama?
DOMAYO: Mimi ni mchezaji wa Yanga na nitabaki kuwa mchezaji wa Yanga, binafsi najipanga vizuri kuyakabili mashindano ya kimataifa ambayo yatanikutanisha na wachezaji wa mataifa mbambali barani Afrika.
FULLSHANGWE: Wenzenu Simba mwaka huu wamekalia kuti la moto, mwaka ujao kazi kwenu, unaonaje?
DOMAYO: Tumeshinda ubingwa, lakini daah! Kazi ipo,  bado tuna changamoto ya kucheza ligi ya mabingwa, kama mnavyojua kule kuna timu nzuri na wachezaji wazuri, usiwe na wasiwasi tutajipanga tu.
FULLSHANGE: Umeionaje ligi kuu msimu huu?
DOMAYO: Ligi ya mwaka huu ilikuwa na changamoto kubwa kutoka kwa timu shiriki hadi kwa mashabiki wa timu ambao siku zote wanahitaji ushindi. Mara nyingi mashabiki wa timu kubwa wanapenda ushindi, mchezaji ukikosea wanachukia, mimi hainipi shida, nachukulia changamoto tu kwani hata ulaya mashabiki ndio wanaochangamsha soka.
FULLSHANGWE: Umeitwa na kocha Kim Paulsen katika kikosi cha Taifa stars, unajisikiaje?
DOMAYO:  Najisikia furaha! Nimefurahi sana!  Unajua kuna vijana wengi wenye uwezo, lakini kocha amekuwa ikinipa nafasi ya kucheza zaidi. Mwalimu ana falasafa yake, kuna wachezaji wengi wanaofaa, lakini kanichagua mimi. Binafasi sitamuangusha hata kidogo.
FULLSHANGWE: Vipi una ndoto za kucheza soka la kimataifa?
DOMAYO: Una uliza ndizi Tukuyu! Naota sana kaka, natamani kucheza soka la kulipwa kama wanavyofanya waliotutangulia, nadhani siku itafika na nitapata nafasi, nazingatia sana nidhamu ya soka.
FULLSHANGWE: Asante sana Frank Domayo kwa ushirikiano wako, kila la heri na hongera sana kwa ubingwa?
FULLSHANGWE: Shukurani sana Anko! Karibu sana na kazi njema kwako, naipenda Fullshangwe.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video