Na Baraka Mpenja kwa Msaada wa Sportsmail.com
Meneja
wa mabingwa wapya wa ligi kuu soka nchini Uingereza, Manchester United ”
Mashetani wekundu”, mskotish Alexndar Chapman Ferguson “Kibabu Fergie”
atakosa mwanzo wa msimu ujao wa ligi hiyo wakati timu yake itakapoanza
kampeni ya kuutetea ubingwa wake kutokana na mipango ya kwenda kufanyiwa
upasuaji msimu wa kiangazi barani ulaya.
Haijabanishwa
wazi kuwa Fergie mwenye miaka 71 kwa sasa atafanyiwa upasuaji sehemu
gani, lakini ametajwa kuwa na matatizo ya kiafya mara kadhaa na njia
pekee ni kufanyiwa upasuaji.
Huduma
hiyo ya kiafya itafanyika wakati klabu ya United ikiwa tayari
imesharejea nyumbani kutoka katika ziara ya maandalizi ya msimu wa ligi
kuu soka Uingereza msimu wa 2013/2014.
United
itarudi England siku 18 kabla ya kuanza kwa msimu mpya na inasemekana
muda huo hautatosha kwa kocha wake kurudi kazini mara moja kutokana na
zoezi hilo.
United
wamethibitisha kuwa meneja huyo aliyewaongoza kutwaa ubingwa wa 20
mwaka huu atafanyiwa upasuaji huo lakini zoezi hilo halina madhara
katika nafasi yake kwani itabaki pale pale.
Katika
maandalizi ya msimu mpya wa ligi kuu England, mipango ya United ni
kufanya ziara ya wiki tatu katika nchi ya Thailand, Austria, Japan na
Hong Kong na kurejea julai 30 mwaka huu ili kujandaa na mechi ya
ufunguzi kati ya Man city au Wigan Agosti 11.
Siku zote Ferguson huwa anasema afya yake ndiyo itabainisha anakaa Old Traford kwa muda gani
Kibabu Fergie akiwa na kocha wa Arsenal, mzee Arsene Wenger kwenye moja ya mechi ya Man U na Arsenal
Mzee kibabu hana mipango ya kujiuzulu hata baada ya kuipa united ubingwa wa 20 mwaka huu.
0 comments:
Post a Comment