Saturday, May 18, 2013

DSC_0226Mashabiki wa Yanga leo hii uwanja wa Taifa wakiwa na kombe la bandia kabla ya mwari wenyewe

Kabla hatujaangazia kipute cha watani wa jadi, Simba na Yanga, MATUKIO DUNIANI ikujulishe matokeo ya mechi nyingine zilizopigwa leo hii.
Toto African tayari wameshashuka daraja licha ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya maafande wa Ruvu shooting kutoka mkoani Pwani katika dimba la CCM kirumba Mwanza.
Mgambo wamefanikiwa kubaki ligi kuu baada ya leo hii kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Africa Lyon katika uwanja wa CCM Mkwakwani Tanga.
JKT Ruvu chini ya kocha Keny Mwaisabula wameshinda bao 1-0 dhidi ya Mtibwa Sugar katika uwanja wa Chamazi.
Wajela jela Tanzania Prisons wamefungwa bao 1-0 na Kagera Sugar katika uwanja wao wa nyumbani wa Sokoine mkoani Mbeya.
JKT Oljoro wamefungwa bao moja kwa bila na Azam fc katika uwanja wa Sheik Amri Abeid Kaluta  jijini Arusha.
Matokeo ya leo yanamaanisha, Africa Lyon, Toto Africans ya Mwanza na Polisi Morogoro zimeporomoka daraja na kuzikaribisha timu za Mbeya City, Rhino Rangers na wauza Mitumba wa Ashanti United.
Sasa turejee katika kipute cha aina yake kilichopigwa jijini Dar es salaam uwanja wa taifa baina ya watani wa jadi Simba na Yanga.
Mabingwa wa ligi kuu bara msimu huu, Dar Young Africans wameongeza furaha yao zaidi leo hii baada ya kuwaadhibu Simba mabao 2-0.
Mabao ya Yanga yamefungwa na Didier Kavumbagu dakika ya tano ya kipindi cha kwanza na msumari wa pili umefungwa na Hamis Kiiza “Diego” katika dakika ya 63 akitumia makosa ya mabeki Cholo na Mude walioshindwa kuosha mpira langoni mwao.
Mbali na ushindi huo, mechi hiyo pia imetumika kugawa zawadi kwa washindi wa ligi kuu Vodacom Tanzania bara msimu huu.
Uwanjani yametokeo matukio ya aina yake, moja ni Mwamuzi wa mchezo Martin Saanya kutoka Morogoro kupata ajali ya uwanjani baada ya kugongwa na kipepsi cha mchezaji na kupasuka sehemu ya jicho dakika za lala salama.
 Pia katika dakika ya 26 Musa Mude alikosa penati waliyozawadiwa na Saanya baada ya Canavaro kumfanyia madhambi Mrisho Ngasa katika eneo la hatari.
Kipa Ally Mustapha “Bartez” alidaka shuti hafifu ama dhaifu alilopiga Musa Mude
Pia Kituko kilitokea baada ya Canavaro kumzonga mwamuzi kama alivyofanya msimu uliopita katikka mchezo dhidi ya Azama FC ambapo walifungiwa kwa kumpiga mwamuzi Israel Nkongo.
Dakika ya 85 kipindi cha pili, Nizar Halfani alipiga shuti kali na la mwaka ambapo baada ya kugonga mwamba wa chini lilimgonga kipa Juma Kaseja sehemu ya paji la Uso na kulala kwa muda wa dakika kadhaa.
Mchezaji wa timu ya Yanga Didier Kavumbagu akikokota mpira mbele ya mchezaji wa timu ya Simba Abdallah Seseme katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom unaofanyika jioni hii kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam , hivi sasi ni kipindi cha pili na Yanga wanaongoza magoli 2 -0 dhidi ya Simba ambayo imekosa penati katika kipindi cha kwanza wakati mchezaji wake Mussa Mude akipiga vibaya mpira huo baada ya Mrisho Ngassa wa Simba kuangushwa kenye eneo la hatari _MG_0386 
Wachezaji wa timu ya Simba na Yanga wakiwania mpira wakati wa mchezo wao unaofanyika kwenye uwanja wa Taifa jioni hii. _MG_0398 
Baada ya golikipa wa Simba Juma K. Juma kuteswa hali ilikuwa hivi. _MG_0401 
Wachezaji wa Yanga wakishangilia baada ya kupata goli la kwanza dhidi ya Simba.

Baada ya mechi kumalizika, makocha wa timu zote waliongea na waandishi wa habari.
Ernie Brandts kocha wa Yanga alisema “ushindi huu ni wa timu yote, niliwaambia wachezaji kabla ya mechi kuwa tunatakiwa kushinda kwa ajili ya mashabiki na viongozi wetu, mafanikio haya ni kutokana na ushirikiano mzuri tunaopewa na mwenyekiti wetu Manji na makamu bwana Sanga”.
Kocha Simba Patrick Liewig alisema “ni sawa kupoteza mchezo, wamestahili kushinda kutokana na mchezo mzuri, sina shaka, lakini wachezaji wangu hasa sehemu ya ulinzi wamenighraimu sana, ukiangalia mabao yote yamefungwa kutokana na uzembe”.
Wakati wa kugawa zawadi, kuna matukio ya aina yake ya kufurahisha na kuhuzunisha pia.
Kitebndo cha wachezaji wa Simba kutokeo mbele ya mgeni rasmi wakiwa wamevalia majinsi yao, malapa, na singalendi, hakika limeshangaza wengi na ukizingatia mchezo huo ulikuwa unatazamwa na watu wengi zaidi duniani kutokana na kurushwa na Supersport. kama ilikuwa sahihi kufanya vile, unatakiwa kuangalia wenzetu wa majuu wakati wa kupokea zawadi wanavaliaje.
 Suala la pili ni kitendo cha Jerryson Tegete kushangilia  akiwa amebeba kombe huku akivalia jezi nyekundu ya Simba aliyobadilishana na mmoja wa wachezaji wa Simba.
Tukio lingine ni kitendo cha Ngasa kubebwa na mshabiki wa Yanga huku akiwa amevalishwa jezi ya Yanga wakati ni mchezaji wa Simba.
Haya ni baadhi ya matukio muhimu ambayo tumeyabaini katika mchezo huu.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video