Thursday, May 2, 2013


Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe Dar es salaam
Siku moja baada ya kutetea ubingwa wake wa IBF Afrika mbele ya mpinzani wake,  mtu wa watu Thomas Mashali “Simba asiyefugika” katika ukumbi wa PTA usiku wa jana, bondia ambaye kwa sasa hana mpinzani nchini Tanzania, mkazi wa mji kasoro bahari , Morogoro, Francis Cheka amesema siku zote nidhamu kubwa ya kufuata maelekezo ya waalimu wake,  kuzingatia mazoezi na kutambua umuhimu wa kutunza afya yake ndii siri ya mafanikio yake ulimwengu wa masumbwi
Cheka ameiambia MATUKIO DUNIANI  kuwa ushindi wa jana ni zawadi kwa wakazi wa Morogoro ambao siku zote ni mashabiki wake wakubwa wakati wake huu wa maisha ya ndonga.
“Nilisema toka awali kuwa nahitaji kushinda pambano hilo, mashabiki wangu walinitaka kutetea ubingwa wangu, kwa kuzingatia maoni yao nilijipanga kama kawaida yangu na kilichotokea jana nilijua tu”. Alisema Cheka.
Bondia huyu mwenye ngumi kali kwa wapinzani wake aliongeza kuwa mabondia wa Tanzania wana majina makubwa kwa vyombo vya habari na wana maneno mengi, lakini yeye siku zote ni kuonesha vitendo tu
“Mie sio msemaji sana ndugu yangu, unajua wengi wanasema sana wanapojiandaa kukutana na mimi, lakini wanaangukia pua, Mashali alitamba sana na akasema lazima amalize ufalme wangu wa sasa, nilitambua hilo nikamfanyia mazoezi na hatimaye imefahamika”. Alisisitiza Cheka.
Cheka alisema mpinzani wake ambaye ni bingwa mtetezi kwa ukanda wa Afrika Mashariki na kati alicheza kwa kiwango kizuri tofauti na michezo yake mingine, lakini kushindwa kwa “Nock Out” alistahili kutokana na uwezo wake kuwa mdogo mbele yake.
“Cheka atabaki kuwa cheka, amini usiamini mimi niko fiti sana, mashabiki wangu wanajua hilo na ndio maana wanajenga imani kubwa na mimi”. Alisema Cheka.
Baada ya kuibuka na ushindi huo jana katika ukumbi wa PTA jijini hapa, Cheka alizawadiwa gari aina ya Noah ambayo iliandaliwa rasmi na IBF Africa.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video