Monday, May 20, 2013

Habari hii imeandikwa na Baraka Mpenja, mmiliki wa blog hii na mwandishi wa mtanado wa FULLSHANGWE

Beki wa Yanga Nadir Haroub “Canavaro” aliyeshika mwari baada ya kutangazwa rasmi mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara uwanja wa taifa 


Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe Dar es salaam
Habari ya mjini bado nii ubingwa wa 24 wa Yanga ambao waliutwaa mapema kabla ya ligi kumalizika, lakini furaha kubwa imekuja baada ya kuwafunga watani zao wa jadi Wekundu wa Msimbazi Simba mabao 2-0 katika dimba la taifa jijini Dar es salaam.
Jana tulikuwa na mahojiano maalumu na kiungo kinda wa klabu ya Yanga, Frank Domayo, leo hii mtandao huu umekutana na nahodha wa mabingwa hao wa ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2012/2013, Mzanzibar Nadir Haroub “Canavaro” na mahojiano yameenda ifuatavyo.
FULLSHANGWE: Nahodha wa Yanga Nadir Haroub “Canavaro” umeiongoza klabu yako kutwaa ubingwa wa 24, unajisikiaje?
CANAVARO: Aisee! nauchukulia kwa furaha kubwa sana, kiukweli mchezo ulikuwa mzuri sana, tulicheza vizuri na kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Watani wetu wa jadi Simba.
FULLSHANGWE: Yanga mlistahili ushindi?
CANAVARO: Kiukweli tulistahili, toka mwanzo wa mchezo mpaka mwisho tulicheza vizuri sana, Simba walicheza kwa muda mfupi. Sisi tuliingia kwa lengo la ushindi tu na tulicheza kuutafuta kufa na kupona ili kufurahia ubingwa wetu na mashabiki wetu, tumefanikiwa!.
FULLSHANGWE: Wewe ni nahodha wa Yanga, siri ya kucheza vizuri zaidi ya Simba ilikuwa nini?
FULLSHANGWE: Kikubwa ni umoja wa wachezaji wa Yanga, nimewaongoza na kuwasihi tucheze kutafuta ushindi,wamenielewa vizuri. Ukumbuke tukiwa Pemba tulifanya mazoezi kwa umoja mkubwa tukifirikia sana ushindi na tumewashinda Simba.
FULLSHANGWE: Unawazungumziaje Simba?
CANAVARO: Simba ni timu nzuri, ina wachezaji wazuri, binafsi nawaheshimu sana ila jana tuliwazidi sana na huo ndio mpira wa miguu, lazima ukubali matokeo. Tuliwazidi kila Idara na hatuwapa nafasi zaidi ya penati waliyopapa ingawa kipa wetu alicheza na tukaendelea na mchezo.
FULLSHANGWE: Baada ya mwamuzi Martin Saanya kutoa Penati ulimzonga sana, kwanini?
CANAVARO: Sidhani kama ilikuwa sahihi, Mwamuzi ndio mtu wa mwisho na mimi ni mchezaji, nitalalamika tu, lakini mwamuzi ndio mwisho. Mchezaji huna ujanja mwamuzi atakapofanya maamuzi, nilikubali penati na kipa wetu akaicheza vizuri sana.
FULLSHANGWE: Ulipewa Shampeni uifungue, baada ya kufanya hivyo ukainywa, unapenda pombe?
CANAVARO: Daah! Sielewi nini kilitokea, mimi sio mlevi wala mvuta sigara, nilijikuta kunywa baada ya furaha kuzidi. Leo hii nimemuomba msamaha mama yangu kwa kitendo kile, nimekubali furaha inaweza kukusababisha ukatenda dhambi na kumkosea Mungu, nimemuomba Mungu msamaha kwasababu mimi sio mlevi wa pombe
FULLSHANGWE: Wewe haunywi pombe kabisa?
CANAVARO: Sijawahi kunywa pombe na watu wanajua, furaha inapozidi mipaka inaweza kukughraimu, nashangaa kwa kweli, Mungu namuamini sana, namtanguliza mbele, anisamehe sana.
FULLSHANGWE: Ukikaa nafasi ya ulinzi huwa unaosha mipira bila kuremba, kwanini huwa una maamuzi ya haraka namna ile?
CANAVARO:  Duniani kote beki hasifiwi, unaweza kucheza vizuri na kupaka rangi mipira na ukafanya kosa moja kuifungisha timu yako, utalaumiwa zaidi ya ulivyocheza vizuri, mimi maamuzi yangu ni ya haraka sana, na ndio sifa yangu kubwa. Hakika maamuzi kama yale huwa yananisaidia sana kutoigharimu timu yangu.
FULLSHANGWE: Baada ya hapa unajiunga na timu ya taifa, unajisikiaje kutajwa na kocha Kim Paulsen katika kikosi cha Taifa stars?
CANAVARO: Nimefurahi sana! Suala la timu ya taifa ni maamuzi ya mwalimu, cha msingi namshukuru kocha kuniita. Timu ya taifa ni ya watu wote, mtu mwenye sifa anatakiwa kuichezea, kikubwa ninawaomba Watanzania watuunge mkono katika safari hii ya kuelekea Brazil mwakani, hatutawaangusha hata kidogo.
FULLSHANGWE: Asante sana Canavaro kwa ushirikiano, tutawasiliana zaidi!
CANAVARO: Asante sana kwa kunipa nafasi, wape salamu wana Yanga na karibu sana.
FULLSHANGWE: Asante na kila la heri!

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video