Saturday, May 25, 2013

Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com

LEO NDIO LEO Uwanja wa Wembley Jijini London kuanzia Saa 3 Dakika 45Usiku wakati Klabu za Ujerumani , Mabingwa wa Nchi hiyo Bayern Munich na Mabingwa wa Msimu uliopita Borussia Dortmund, watakapocheza Fainali ya UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI, ambapo Mshindi ndie rasmi Klabu Bingwa ya Ulaya.
Meneja wa Borussia Dortmund Jurgen Klopp anaamini Fainali hii ya kwanza kuzikutansha Klabu za Germany ni kitu spesho na amesema: “Klabu hii ingeweza kusambaratika. Badala yake tumefufuka toka kwenye majivu. Hii ni Gemu spesho katika sehemu spesho dhidi ya Mpinzani maalum! Kama hii ndio Fainali yangu pekee maishani mwangu na nikifa nikiwa na Miaka 60 basi haitakuwa mbaya!”
Klopp, akiongelea kusambaratika, alikuwa akimaanisha Mwaka 2005 ambapo nusura Klabu hiyo itangazwe mufilisi.
Borussia Dortmund watatinga Fainali hii bila Kiungo wao Chipukizi na hatari, Mario Gotze, ambae ni majeruhi lakini pia pengine hilo ni heri kwao kwani hii ingekuwa ni Mechi yake ya mwisho kwao kwani anahamia Bayern Munich kwa ajili ya Msimu ujao.
Akiongezea, Klopp, mwenye Miaka 45, alinena: “Soka ni Dini kwa Dortmund.
Bayern Wanaweza kuwa na Mashabiki wengi na kushinda Mataji mengi, lakini sasa ni hadithi nyingine. Sasa imekuja Klabu nyingine ambayo ni nzuri pia. Tunazo pesa za kupata Wachezaji wazuri. Lakini zipo Klabu nyingine zinaweza kutumia pesa nyingi zaidi. Sisi tunachulkua msimamo tofauti!”
Lakini Kambi ya Mabingwa wa Germany, Bayern Munich, ipo na morali kubwa kupita Msimu uliopita walipofungwa Fainali ya UCL na Chelsea kwa Mikwaju ya Penati.
Mwaka 2010, Bayern pia walifungwa Fainali ya UCL na Inter Milan kwa Bao 2-0.
Akiongelea hali hii, Mchezaji wa Bayern, Thomas Muller, amesema: “Borussia ni Timu kamili. Hivyo ni ngumu kucheza nayo kupita Timu ya Wachezaji binafsi. Lakini sidhani kama tuna udhaifu. Tumecheza Gemu nyingi na hatujafungwa Bao nyingi. Ninajisikia vyema na nahisi tutapata matokeo mazuri!”
Kwenye Mashindano haya, Bayern wamesonga toka hatua ya Makundi kwa kishindo ingawa walisota walipocheza na Arsenal kwenye Raundi ya Mtoano ya Timu 16 na kuitoa tu kwa Sheria ya Magoli ya Ugenini.
Lakini baada ya hapo walizisambaratisha Juventus na Barcelona kwa kuzinyuka Jumla ya Mabao 11-0 huku Barcelona wakitupwa nje ya Nusu Fainali kwa kutandikwa Bao 4-0 na 3-0 katika Mechi mbili.

Visitor: Dortmund coach Jurgen Klopp (left) at Wembley with Aston Villa manager Paul Lambert, who won the Champions League with the German club in 1997
Ugeni: Kocha wa Dortmund, Jurgen Klopp (kushoto) akiwa Wembley na kocha wa Aston Villa, Paul Lambert, ambaye aliiwezesha klabu hiyo ya Ujerumani kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa mwaka 1997
Deep discussion: Bastian Schweinsteiger, Arjen Robben and Franck Ribery at Wembley
Tutawamaliza vipi?:Bastian Schweinsteiger, Arjen Robben na Franck Ribery wakiwa Wembley
Tunnel walk: Bayern Munich players walk out onto the Wembley pitch for a training session
Wachezaji wa Bayern Munich wakiingia Wembley kufanya mazoezi jana
Running repair: Prolific Dortmund striker Robert Lewandowski gets his boot fixed
Anarekebishwa: Mshambuliaji tegemeo wa Dortmund, Robert Lewandowski akirekebishiwa viatu vyake
Das boot: A close-up of Lewandowski's boot for the final
Kiatu cha mabao: Kiatu cha Lewandowski fainali
Grappling: Kevin Groskreutz, Robert Lewandowski and Marco Reus warm up for training
Utatu mtakatifu: Kevin Groskreutz, Robert Lewandowski na Marco Reus wakiwa mazoezini Wembley jana

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video