Saturday, May 4, 2013

RAFAEL BENITEZ: KOCHA BORA WA MWEZI APRIL 2013.

Shirikisho la mpira wa miguu nchini UINGEREZA FA, limemtangaza meneja wa muda wa klabu ya CHELSEA , RAFAEL BENITEZ kuwa kocha bora wa mwezi wa Aprili msimu huu kwenye ligi kuu ya nchini humo baada ya timu yake  kushinda michezo mitatu mfululizo dhidi ya  Sunderland, Fulham na Swansea, huku ikitoa sare ya magoli 2-2 dhidi ya klabu ya LIVERPOOL  kwenye mchezo uliopigwa dimbani ANFIELD  mwezi uliopita.
Rafael Benitez
Akiongea kupita mtandao wa klabu hiyo  hiyo BENITEZ amesema siri ya mafanikio katika klabu yake ni umoja na ushirikiano wa hali ya juu uliopo kati ya wachezaji , kocha na viongozi wa timu kwa ujumla huku akisisitiza kuwa licha ya kushindwa kunyakua ubingwa wa ligi kuu nchini Uingereza msimu huu, bado timu yake ina nafasi kubwa ya kufanya vizuri kwa msimu mwingine  ujao kwani  kwa sasa wako katika  nafasi nzuri  kwenye msimamo wa ligi ligi.
Hata hivyo Chelsea ambao wamejihakikishia tiketi ya kucheza fainali ya kombe la shirikisho barani ulaya baada ya hapo juzi  kuwatandika FC BASEL  magoli 3-1 dimbani Stamfordbrige, kwa sasa wako nafasi  ya tatu alama  moja mbele ya Arsenal  kwenye msimamo wa ligi huku wakiwa wamebakiwa na michezo minne  mkononi.


ARSENE WENGER;NINA MAPENZI YA KWELI NA ARSENAL.


Kocha wa klabu ya ARSENAL , ARSENAL  WANGER  leo ameweka wazi kuwa  anapenda  kubaki dimbani EMMIRATE kuendelea kufundisha klabu yake  ya sasa licha ya kuwepo na tetesi kuwa  klabu ya PARIS SAINT GERMAIAN ya huko nchini Ufaransa  inamipango ya  kumsajii  mwishoni mwa msimu huu.

WENGER ambaye timu yake inang’ang’ana kubaki kwenye nafasi ya  nne bora kwenye msimamo wa ligi kuu nchini Uingereza, akiongea na wanahabari amesisitiza kuwa ana mapenzi makubwa na klabu ya Arsenal, hivyo haoni sababu ya kuhamia klabu nyingine kwa sababu ya pesa huku akisaliti klabu yake anayoipenda  kwa moyo.
Arsene Wenger - Arsenal Training Session & Press Conference
Kusho, Arsene Wenger, Jack Wilshere wakijadili jambo mazoezini.
Aidha WENGER ameongeza kuwa licha ya klabu yake kupita katika kipndi kigumu cha ligi, bado anaamini timu yake iko katka nafasi nzuri  kwa ajili ya msimu mwingine ujao.
MOURINHO: REKODI YANGU INAJIELEZA YENYEWE. 

Kocha wa klabu ya  REAL MADRID  JOSE MORINHO  mapema leo akiongea na wanahabari, amesema kuwa  ni vyema  watu wamzungumzie  kwa kutumia kigezo cha mafanikio alionayo kuliko kutumia kutumia  kigezo cha kushindwa kuchukua ubingwa kwenye   michuano ya klabu bingwa barani Ulaya.

Mourinho: My record speaks for itself
Jose Mourinho.
MORINHO mwenye asili ya nchini  URENO, aliwahi kushinda mataji  manne katika nchi nne tofauti , lakini pia ni miongoni mwa makocha watatu pekee waliowahi kunyakuwa ubingwa wa  CHAPIONS LEAGUE  akiwa na timu mbilli tofauti.

Hata hivyo kibabu huyo ambaye kwa sasa anahusishwa  na taarifa za  kuhamia klabu yake ya zamani ya CHELSEA mwishoni mwa msimu huu, ameendelea kusitiza kuwa  rekodi ya ligi bado inabaki kuwa yake licha ya mambo kumuendea kombo msimu huu  kwenye hatua ya nusu fainali ya klbu bingwa baada ya kutolewa nje ya michuano hiyo  na klabu ya BORUSSIA DORTMUND kwa tofauti ya goli 1-0
Kivuyo Francis         www.goal.com

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video