Friday, May 17, 2013

Tangu alipoingia Chelsea kama kaimu mkufunzi Rafael Benitez amekuwa na wakati mgumu kwani mashabiki wa Stamford Bridge  wamekuwa hawampendi.
Lakini baada ya kuifunga Benfica mashabiki hao hao ambao walikuwa hawampendi Benitez waliishangilia ushindi wa timu yao kwa vifijo na nderemo huku wakisahau chuki waliokuwa nao kwa kaimu meneja huyo.
Hatimae kocha Mhispania  Rafael Benitez ataondoka Chelsea akiwa na tabasabu baada ya timu yake kubeba ubingwa wa Kombe la Europa League kwa kuifunga timu ya Benfica ya Ureno 2-1 usiku wa Jumatano katika uwanja wa Amsterdam, Uholanzi.
Hii ni baada ya Branislav Ivanovic kufunga bao la pili  maridadi kwa kichwa wakati dakika za  majeruhi wakati mashabiki wakiamini mechi ingeongezwa dakika 30 za nyongeza na pengine ingeamuliwa kwa mikwaju ya penati ya piga nikupige,lakini haikuwa hivyo.
Mwaka jana Chelesea ilishinda Kombe la Klabu bingwa bara Ulaya na mwaka huu wamebeba kombe la Europa League.
Bao lakwanza la Chelsea lilifungwa na mshambulizi Fernando Torres nao Benfica wakapata lao kupitia mwaju wa penalti uliofungwa na Oscar Cardozo.
Ushindi wa Chelsea unamfanya Rafael Benitez kuwa meneja wa nne kushinda kombe la Klabu Bingwa Uropa na la Europa League zaidi ya mara mmoja.
Wengine amabo wamewahi kushinda kumbe hilo zaidi ya mara moja ni Giovanni Trapattoni: 1977 (Juventus); 1991 (Inter); 1993 (Juventus) ,Luis Molowny: 1985 & 1986 (Real Madrid) Juande Ramos: 2006 & 2007 (Sevilla).

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video