Wednesday, May 1, 2013

GWIJI wa soka Colombia, Faustino Asprilla amesema kwamba amemuambia Radamel Falcao asaini Manchester United.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27 wa Atletico Madrid amekuwa gumzo kuelekea dirisha la usajili, akiwaniwa na klabu kadhaa zikiwemo Chelsea na Manchester City pia.
Lakini mshambuliaji wa zamani wa Newcastle, Asprilla anaamini nyota huyo mwenye thamani ya Pauni Milioni 46 anaweza kutua Old Trafford msimu ujao.
Perfect fit? We imagine how Radamel Falcao would look in a Manchester United shirt
Atapendezaje? Fikiria vipi Radamel Falcao ataonekana katika jezi ya Manchester United
Wanted man: Radamel Falcao is set to be in demand this summer as the race for his signature hots up
Anawaniwa: Radamel Falcao

Asprilla amesema: "Tulizungumza na aliniuliza mimi maoni yangu aende timu gani. Anafahamu kwamba kila klabu kubwa duniani inamtaka. NI mchezaji asiyehadaika na fedha -  anachotaka ni sehemu ambayo familia yake itafurahia  na ambako atapata mafanikio. 
"Na timu kama Real Madrid, PSG, Manchester City zina wakati mzuri kuliko zinavyokuwa na wakati mbaya - na ndiyo maana nikamuambia lazima achague Manchester United. Kila msimu wanapigana - na ikiwa anataka mafanikio huko ndiko ambako nimemuambia aende.
Asprilla anaamini Falcao atakuwa mchezaji pekee daima kucheza Ligi Kuu ya England ambaye anaweza kufanya vitu kama Alan Shearer. 
"Ni vigumu kwangu kufafanua ni mzuri kiasi gani - ni mmaliziaji mzuri zaidi duniani. Mchezaji pekee aliyecheza Ligi Kuu England ambaye ana kiwango chake cha umaliziaji ni Alan Shearer. 
"Ikiwa atasaini Manchester United - atawasaidia kupata taji la Ligi ya Mabingwa. Robin van Persie na Radamel watakuwa hawakamatiki,".
Deadly: Falcao has been unstoppable in front of goal during his time at Atletico Madrid
Muuwaji: Falcao amekuwa hakamatiki anapokuwa mbele ya  mdomo wa lango Atletico Madrid

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video