Na Baraka Mpenja wa kwa msaada wa Sportsmail.com
KLABU
ya Arsenal itaiwakilisha London Kaskazini katika Ligi ya Mabingwa msimu
ujao baada ya kushika nafasi ya nne katika msimamo wa Ligi Kuu ya
England – lakini Tottenham wamebaki na maumivu baada ya kuamini
walinyimwa penalti za wazi White Hart Lane.
Timu
ya Arsene Wenger, Arsenal imetinga Ligi ya Mabingwa kwa mara ya 16 na
kujipatia kitita cha Pauni zisizopungua Milioni 25, baada ya kuifunga
Newcastle 1-0 bao pekee la Laurent Koscielny dakika ya 51 Uwanja wa St
James Park. Sunderland nayo ilishinda 1-0, dhidi ya Sunderland bao pekee
la Gareth Bale dakika ya 89.
Laurent
Koscielny aliifungia Arsenal Bao pekee na la ushindi katika Dakika ya
52 na kuipa Arsenal Nafasi ya 4 na hivyo kucheza UCL Msimu ujao.

Sherehe ya timu: Arsenal wakishangilia na mashabi wao katika dimba la St James Park baada ya kupata ushindi

Msimamo wa timu za juu baada ya michezo ya leo

Nao
Tottenham Hospurs leo hii wamepata nafasi ya kucheza ligi ya Uropa
msimu ujao baada ya kushinda mchezo wa leo huku Gareth Bale.

Bale akifunga bao lake alilofunga leo hii, lakini halijatosha kuwapa nafasi ya kucheza ligi ya mabingwa barani ulaya msimu ujao

Bale akishangilia bao lake linaloiwezesha Spurs kucheza Europa League msimu ujao

Mamilioni ya Euro: Beki wa Arsenal, Laurent Koscielny akiifungia timu yake bao pekee Uwanja wa St James Park


Cazorla akiwapongeza wenzake

0 comments:
Post a Comment