Saturday, May 25, 2013


160

Na Baraka Mpenja 
Baada ya kuporomoka daraja msimu wa ligi kuu soka Tanzania bara uliomalizika mei 18 mwaka huu, maafande wa Polisi Morogoro wamesema wamewapa mapumziko ya wiki mbili wachezaji wao na baada ya hapo watarudi kambini kuweka mikakati ya kurudi ligi kuu msimu wa 2014/2015.
Afisa habari wa klabu hiyo Clemence Banzo ameimbia MATUKIO DUNAINI Kuwa wameamua kuwabakisha wachezaji wao wote ili kuhakikisha ndani ya mwaka mmoja wanarudi ligi kuu na kuendelea kutoa burudani kwa mashabiki wa kandanda mjini Morogoro.
“Kushuka daraja haikuwa mipango yetu, tulikosa sapoti kutoka kwa wadau na viongozi wa jeshi kitaifa, lakini kama tutabahatika kurudi  ligi kuu, hakika tutazungumza na viongozi wetu wa wizara ili waisaidie timu moja ya polisi kupata msaada” .Alisema Banzo.
Akizungumzia ushindani wa timu za majeshi michuano ya ligi, Banzo alisema timu hizo zinajitahidi sana ingawa kuna changamoto za kifedha.
Banzo alisema baadhi ya timu hizo zinasaidiwa sana huku akitolea mfano klabu ya Tanzania Prisons ambayo hupewa msaada kila mkoa inapoenda kucheza mechi.
Afisa habari huyo aliongeza kuwa kwa sasa kuna haja kwa jeshi la Polisi Tanzania kutengeneza timu nzuri ya kuliwakilisha jeshi hilo kitaifa na kimataifa kama nchi nyingine.
“Tunakosa misaada sana kwa kweli, imekuwa ngumu sana kuendesha klabu yetu, kama sio wadau wa soka mkoani Morogoro tungekuwa na hali ngumu sana, lakini tanajipanga vizuri kurejea ligi kuu bara”. Aliongea Banzo kwa kujiamini.
Kuhusu kocha wao Rishard Adolf, Banzo alisema wapo katika mazungumzo na kocha huyo ili aendelea kuifundisha klabu yake na airudishe ligi kuu kwa mara nyingine.
“Adolf ametusaidia sana na ndio maana baada ya kuchukua timu msimu wa pili alifanya vizuri sana, alijenga morali ya wachezaji na kupata matokeo mazuri, tunadhani hakuna haja ya kumuachia kocha huyo mwenye uezo mkubwa”. Alisema Banzo.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video