Wednesday, April 24, 2013

Mabingwa wa ligi ya Bundesliga ya nchini ujerumani, The Bavarian Bayern Munich wameanza vyema kampeni ya kuelekea kucheza fainali ya tatu ya Ligi ya Mabingwa barabi Ulaya ndani ya miaka minne, baada ya kuwazamisha bila huruma wale wanaodaiwa kuwa bora zaidi kuwahi kutoka katika hii dunia, Wakatalunya FC   Barcelona mabao 4-0 usiku huu kwenye Uwanja wa Allianz Arena katika Nusu Fainali ya kwanza.

Mabao mawili kutoka kwa Thomas Muller na moja kwa kila mmoja, Mario Gomez na Arjen Robben yamempa faraja kocha Jupp Heynckes ambaye sasa sijui itokee miujiza gani Jumatano ijayo Uwanja Nou Camp kwenye mchezo wa marudiano akose tiketi ya kwenda Wembley.
Katika mchezo huo wa kukata na shoka na uliovuta hisia za mamilioni ya mashabiki wa soka duniani ulianza kwa vijana wa Munich kucheza soka la kasi na nguvu kama ilivyokwaida yao.
Bayern walionesha kuwa na morali kubwa zaidi ya kuhitaji matokeo ya ushindi mbele ya “Catalan Boys” wanaosifika kwa soka la pasi fupi fupi za na za uhakika zaidi.
Kipigo cha jana ni adimu sana kwa Barca kwa siku za karibuni lakini jana hawakuwa na jinsi kutokana na uwezo mkubwa wa wapinzania wao.
Labda miijuza ya soka isubiriwe huko Hispania kama wataweza kupindua kipigo hicho kwa misumari minne kwa ubuyu.
Wakati Bayern wakingara zaidi Allianz Arena, Nyota wa Barca Lionel Andrew Jorge Messi alibanwa mpaka alitia huruma katika mchezo huo.
 
Kikosi cha Bayern Munich kilichofanya mauaji hayo kilikuwa: Neuer, Lahm, Boateng, Dante, Alaba, Javi Martinez, Schweinsteiger, Robben, Muller/Pizarro dk83, Ribery/Shaqiri dk88 na Gomez/Gustavo dk71.
Barcelona: Valdes, Dani Alves, Pique, Bartra, Jordi Alba, Xavi, Busquets, Iniesta, Sanchez, Messi na Pedro/Villa dk83.
Going ahead: Thomas Mueller celebrates giving his side the lead
Fundi mwenye shabaha na akili ya kandanda Thomas Mueller akishangilia baada ya kutia kimiani bao la kwanza
One foot in the final: Bayern Munich's Mario Gomez and team mate Javi Martinez celebrate after going 2-0 up
Fainali hiyooooo!:  Nyota wa Bayern Munich, supa  Mario Gomez na mchezaji mwenzake, mtaalamu Javi Martinez wakishangilia baada ya kupata bao la pili
Remember the name: Robben celebrates in front of the fans after his goal
Winga machachari na mwenye kasi kama mshale Mholanzi Ajen Robben akishangilia mbele ya mashabiki baada ya kufunga bao lake
Feeling down: Barcelona forward Lionel Messi looks dejected
Huruma: Mwanasoka bora wa dunia mara nne mfulullizo wa FIFA raia wa Argentina na mshambuliaji wa Barca, Lionel Andrew Jorge Messi akionekana aliyekata tamaa
No way back? Messi and Barcelona face an uphill task in the second leg
 Messi na Barcelona wanakabiliwa na mchezo mgumu wa marudiano kutokana na ubora walionao The Bavarian Bayern Munich mabingwa wa Bundes Liga
 
LEO KIVUMBI KINGINE
Leo nusu fainali nyingine inasubiriwa baina ya miamba ya sola nchini Hispani, Real De Madrid chini ya kocha maarufu duniani, Mreno Mario Jose Dos Santos Ferlix Mourinho dhidi ya nyuki wa kaskazini mashariki mwa Ujerumani na wenye machungu ya kupoteza ubingwa wao, Borrusia Dortmund. Mechi hiyo itapigwa nchini Ujerumani na wiki ijayo Santiago Bernabeu.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video